Home » » JAJI AWATAKA MAHAKIMU WATAMBUE KAZI YA MAHAKAMA NI KUTENDA HAKI‏

JAJI AWATAKA MAHAKIMU WATAMBUE KAZI YA MAHAKAMA NI KUTENDA HAKI‏



N a  Walter  Mguluchuma
Katavi
Jaji Mfawidhi wa Mahakama kuu  ya Tanzania  Kanda ya Sumbawanga  Jaji Kakusulo  Sambo  amewataka Mahakimu watambue  kwamba  kazi ya msingi  ya Mahakama  ni kutoa haki
Kauli hiyo aliitowa hapo jana wakati alipokuwa akifungua  kikao cha Baraza  la wafanyakazi  la kanda ya Sumbawanga  lililofanyika katika ukumbi wa idara ya maji Mjini Mpanda Mkoa wa Katavi
Alisema  katiba ya nchi yetu ipo  wazi   na inaeleza kwamba chombo   chenye mamlaka  ya kutoa  haki  ni wajibu wa Mahakama ya Tanzania
Jaji   Sambo  alieleza  kila  Hakimuanaowajibu  wa   atekeleze  malengo   na maagizo  yaliopo  kuhusu  utoaji  haki  yaani  usikilizaji wa  mashauri
Alisema  kwa hiyo   jambo  lolote  linalipelekea  kukwamisha    utoaji wa haki  liogopwe  kama ukoma  na viongozi wa maeneo husika  walishughulikie  haraka
 Alieleza Mahakama  za mwanzo  na vikao vya mahakama  kuu  kwa  kesi za mauwaji  huendeshwa kwa kushilikiana na wazee washauri(wazee wa baraza)
Alisema  hawa waheshimiwe  sana  tuwajali   vinginevyo  mahakama  itashindwa  kuteleza jukumu lake la msingi  endapo  wataamua  kutoshirikiana  vyema na mahakama  au wakigoma
Alisisitiza  kuwa  walipwe posho  zao  haraka  na kwa umaakini  mkubwa  ili kuondoa  malalamiko  yasiyo  na msingi  au ulazima  wa kutokea
Alifafanua kwasasa  Mahakama  haina  tatizo la  ukosefu wa fedha  za kuwalipa  washauri hao  hivyo watumisha ambao wanawaandalia malipo wafanye kazi hiyo  bila kusukumwa
Ni  marufuku  na mwiko  kwa pesa zinazoletwa  kwa ajiri ya  kuwalipa washauri  kuzitumia  kwa shughuli nyingine  yoyote ile  hata ikiwa nzito kiasi gani aliagiza jaji huyo

  
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa