Home » » WATU WATATU WAFARIKI KWA AJALI YA GARI

WATU WATATU WAFARIKI KWA AJALI YA GARI


Na  Walter  Mguluchuma
Katavi
Watu watatu wamekufa hapohapo  na  wawili wamejeruhiwa na kulazwa Hospitalini baada ya Roli walilokuwa wanasafilia kupinduka katika Mlima  Kalutwa Wilayani Mpanda Mkoa wa Katavi
 Ajari hiyo  ambayoililihusisha  Roli aina ya  Scania  yenye Namba za usajiri  T.211 AGF lililokuwa likiendeshwa  na Dreva aliyejulikana kwa jina moja  la  Amri ilitokea hapo jana majira ya saa moja usiku  katika mlima wa Kalitwa  barabara ya kutoka Mpanda kwenda Mkoa wa Kigoma
Kamanda Kidavashari   alisema  mpaka sasa kati ya marehemu  hao  watatu   ameweza kutambulika marehemu mmoja  aliyetambulika kwa jina la  Edrick Ndigimiti (MASABO) 30  Mkazi wa Kigoma
Kwa mujibu  wa Kidavashari miili ya marehemu hao ipo katika chumba cha kuifadhia maiti  katika Hospitali ya Wilaya ya  Mpanda
Alisema  huhudi za  kuwatambua marehemu hao  wawili  ambao bado hawajatambulika  zinaendelea kufanyika  kwa  kuwatafuta  ndugu zao
Kamanda Kidavashari aliwaja majeruhi wawili  wa ajari hiyo  kuwa ni  Dickison Mwangalonga (19)Mkazi wa  Mtaa wa Kotazi  mjini  hapa ambae ameumia  katika sehemu za usoni na  mkono wa kushoto na Mohamed Usoni Mkazi wa Mtaa wa Majengo Mjini hapa ambae  ameumia  mguu wa kulia  mkono wa kushoto na mgongoni
  Alisema majeruhi hao  wamelazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Mpanda  na wanaendelea kupatiwa matibabu  zaidi  na hari  zao  zinaendeleavizuri
Kwa mujibu wa Kidavashari  chanzo cha ajari hiyo  kilitokana  na  mwendo kasi  wa Dreva  ambapo mara baada ya  kutokea kwa ajari hiyo  kutokea  alikimbia kusiko julikana
 Alisema Jeshi la Polisi  linaendelea  na upelelezi  kuhakikisha  linamkamata  mtuhumiwa  wa ajari  hiyo  ili  achukuliwe  hatua za Kisheria

  

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa