Na Walter Mguluchuma
Katavi
Jumla ya
Raia wapya 56,554 waliokuwa Raia
wa Burundi kati ya
62,544 wanaoishi katika makazi ya
Wakimbizi ya Katumba Wilaya ya Mlele
Mkoa wa Katavi wamepatiwa vyeti vya urai wa Tanzania
Hayo
yalielezwa hapo jana na Afisa
Maendeleo ya Jamii toka Ofisi
ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Katavi Ignas Kikwala katika taarifa aliyoisoma kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa
Katavi kwa wakati wa
kikao cha sita cha kamati ya ushauri ya Mkoa wa
Katavi(RCC)kilichofanyika katika ukumbi wa idara ya maji mjini hapa
Alisema Mkoa wa Katavi una kambi mbili za Wakimbizi
ambazo ni Katumba na Mishamo hadi kufikia
Novemba 30 mwaka jana
Makazi ya Katumba yalikuwa na
wakimbizi 76,769 kati hati ya hao 62,544
walikubaliwa kupewa uraia wa Tanzania
Waliokataliwa kupewa uraia ni 2150 wanaopaswa kurejea
Burundi kwa hiari yao toka mwaka jana lakini wamekuwa
wakikwepa kurejea kwao kwa sababu mbalimbali
Alifafanua
wakimbizi ambao hawakusajiriwa 647wakimbizi ambao hawakunyimwa Uraia wala kukataliwa ni 218 na Wakimbizi ambao fomu zao zilikuwa na matatizo ni
ishirini
Kikwala
alisema kwa upande wa Makazi ya
Mishamo Watanzania wapya waliopewa uraia ni
52,594 waliokataliwa ni 1155
wanaopaswa kurejea kwao Burundi kwa
hiari ni 2500 na wamekuwa wakikwepa
kurudu kwa kudhania kuwa na wao watapewa Urai wa Tanzania
Hivyo
kufanya jumla ya Raia
wapya wa Tanzania katika Mkoa wa
Katavi watakaopewa vyeti
vya uraia kuwa ni 115,138
Kwa upande wa wake mkuu wa Makazi ya Wakimbizi
ya Katumba Athumani Igwe alieleza kuwa hadi kufikia Februari 20 mwaka huu
jumla ya Raia wapya
waliokuwa wamepewa vyeti vyao vya uraia ni 56,554 kati ya 62,544 katika Makazi ya Wakimbizi ya
Katumba sehemu ambayo
zoezi la ugawaji wa vyeti
limekamilika kwa sasa
Alisema
raia wapya 3692 hawakupewa vyeti
vyao vya uraia kwa sababu
mbalimbali ambapo wengine walikuwa ni
wagonjwa na wengine walikuwa masomoni hivyo utaratibu wa kuwapatia vyeti vya
uraia unaandaliwa kabla ya zoezi hilo
kukamiika katika Makazi ya Mishamo
Kwa sasa
zoezi hilo la ugawaji wa vyeti
unaendelea katika ya Ulyankulu Mkoa wa Tabora baada ya
kukamilika katika makazi
hayo zoezi litahamia
katika Makazi ya Mishamo Mkoa wa
Katavi na linategemea
kukamilika Apri 30 nwaka huu
Aidha katika kikao hicho Mbunge wa Jimbo la
Mpanda Mjini alishauri kuwa maeneo hayo
yaliokuwa ya Makazi ya wakimbizi
yanapaswa kuwa ni maeneo ya
makazi ya watu kutokana na mahitaji ya ardhi kwa watu kwa sasa
Alisema kwani
kabla ya maeneo hayo ya kuwa makazi 1972
yalikuwa ni maeneo ya hifadhi ya mistu
hivyo Serikali ione nanma ya
kubadili matumizi ya eneo hilo
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
0 comments:
Post a Comment