Home » » MARUFUKU KUISHI KATIKA VYANZO VYA MAJI

MARUFUKU KUISHI KATIKA VYANZO VYA MAJI


Na  Walter  Mguluchuma
Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dkt Ibrahim Msengi ameagiza wakuu wa Wilaya za Mkoa wa Katavi kuakikisha  wanawaondoa watu wote  ambao   wanaoishi kwenye vyanzo vya maji na maeneo amabayo hayakurusiwa kuishi na wakuu wa Wilaya wawasimamie wakurugunzi wao kuhakikisha zoezi hilo linafanikiwa.
Dk Msengi ametoa agizo hilo wakati wa kikao cha ushauri wa Mkoa wa Katavi  kilichofanyika jana kwenye ukumbi wa idara ya maji mjini hapa
Amewataka wananchi wote  kuzingatia sheria,kila Mtendaji lazima asimamie sheria na wawajibike kwa kusimamia sheria zilizopo,wasiwe na woga wa kuwaonea aibu wananchi katika usimamiaji wa sheria.
Kutokana na hilo amewaagiza Wakuu wote wa Wilaya kuwasimamia wakurugenzi kuhakikisha wanasimamia sheria kuwa kuwaondoa wale wote wanaoishi maeneo ambayo ni kinyume cha sheria kwa kuwa wameenda kukaa huko kinyume na sheria kila mmoja lazima afuate sheria, na kila mtendaji awajibike kwa nafasi aliyonayo
Wajumbe wa Kikao hicho wameshauri kuwa  shughuli za kisiasa na za kiutendaji  ni vyema zikatenganishwa ili kufuata sheria katika kutekeleza shughuli za serikali na wananchi wafuate sheria.
Akichangia katika kikao hicho Padri wa Kanisa Katoliki ambaye ni Msaidizi wa Askofu Jimbo la Mpanda Kanisa Katoliki  Padri Patrick Kasomo ameeleza kuwa migogoro mingi ya ardhi na mipaka ya vijiji  inasababishwa na kutanguliza siasa wakati wa utekelezaji wa sheria.
Akashauri kuwa wale waliopewa  mamlaka ya kusimamia sheria na mipaka wanafahamika ni watendaji na siyo wanasiasa,akataja baadhi ya maeneo ambayo wananchi wana migogoro na wameanzisha vitongoji kiholela,akataja kijiji cha Kapalamsenga kuwa kuna migogoro ya mipaka kwenye vitongoji.
Awali Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini Said Alf alishauri wataalam wasiadie kusimamia na kuainisha maeneo ya vijiji nay ale yanayodaiwa kuwa na migogoro iainishwe.
Charles Kanyanda Msaidizi wa Mbunge Jimbo la Katavi alishauri kuwa migogoro ya vijiji serikali ianishe  na kuweka mipaka ili kuondoa migogoro hii, ili kuweza kuepuka.
Naye Mbunge wa Jimbo la Mpanda Magharibi  Moshi Selemani Kakoso alieleza kuwa  migogoro mingi  iliyopo kwenye baadhi ya vijiji wilayani mpanda kwa vijiji kumi vilivyopo kwenye Hifadhi ya wanyamapori ya vijiji  inasababishwa na WMA.
Kakoso alisema mbali ya migogoro hiyo ameeleza kuwa vyanzo vya maji vilivyoko kwenye Kata ya Katuma kata ambayo ni ndiyo vilipo vyanzo vingi vya maji ambavyo ni muhimu na tegemeo la wakazi wa mkoa wa Katavi na Hifadhi ya wanyamapori ya Katavi imevamiwa na wafugaji na kuharibu vyanzo hivyo.
Kwa upande wake Mkuu wa Makazi ya wakimbizi Katumba alieleza kuwa eneo la makazi ya wakimbizi ya Katumba vijiji vimeanzishwa ndani ya makazi hayo kiholela hali ambayo ni uvunjifu wa sheria.
Awali Katibu Tawala wa Mkoa Mhandisi Emanuel Kalobelo  aliwaagiza watendaji wote kuainisha makazi yote holela, na mifugo iliyopo kwenye mkoa ili kufahamu idadi ya wakazi na mifugo iliyokopo katika mkoa na kufahamu idadi ya makazi holela.
Akawata Wakurugenzi    kuhakikisha wanasimamia sheria kuwa kuwaondoa wale wote wanaoishi maeneo ambayo ni kinyume cha sheria kwa kuwa wameenda kukaa huko kinyume na sheria kila mmoja lazima afuate sheria, na kila mtendaji awajibike kwa nafasi aliyonayo.


Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa