Home » » WAUGUZI WATAKIWA KUWA NA LUGHA NZURI WANAPOWAHUDUMIA WAJAWAZITO

WAUGUZI WATAKIWA KUWA NA LUGHA NZURI WANAPOWAHUDUMIA WAJAWAZITO


Na  Walter  Mguluchuma
Katavi
 Wauguzi wa Halmashauri ya Mji wa Mpanda Mkoa wa Katavi wametakiwa kutimiza wajibu wa kazi  yao na wawe wanawatolea lugha nzuri akina Mama wajawazito wanapokuwa wanawahudumia
Wito huo ulitolewa hapo juzi na Makamu  Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Mpanda  Yusuph  Ngasa  wakati alipokuwa akiwahutubia  wauguzi wa kituo cha Afya cha Mpanda Mjini  kwenye afla   fupi ya kupokea  msaada wa vitanda vitano vyenye   vya kujifunglia akina  Mama wajawazito vya thamani ya shilingi milioni tano vilivyotolewa na Benki ya NMB
 Ngasa  alisema  wapo baadhi ya wauguzi wamekuwa  wakiwatolea lugha  za matusi akina Mama wajawazito wanao  kwenda kujifungua   hari ambayo inawafanya akina mama  wajawazito  waache kujifungulia kwenye  vituo  vinavyotowa huduma ya uzazi na kuamua kujifungulia majumbani
 Alieleza    kuwa  endapo Wauguzi watatimiza wajibu wa kazi yao  itawasaidia wao  kupunguza lawama  za akina mama wajawazito  zisizo na lazima
 Alifafanua  ili wauguzi  waweze kupunguza lawama zisizo na lazima   za malalamiko ya  akina Mama wajawazito  njia pekee  ni wauguzi kufanya kazi kwa kutimiza wajibu wa kazi zao
 Alisema  akina Mama wanapaswa kuonewa huruma kwani matatizo mengi  yamekuwa  yakiwakuta wanawake kuliko wanaume kwani wao ndio wanaolea watoto hadi kukua
 Ngasa  alieleza  kuwa  kumekuwa na tabia ya wanaume waliowengi  kukataa kwenda huhudhuria  kiliniki  na wake zao  na matokeo yake wamekuwa wakiwaacha wake zao kwenda peke yao

 Umefika wakati sasa wanaume wabadilike  na wawe na tabia ya kwenda  kiliniki  na wake zao  ili waweze  kufahamu maendeleo ya afya ya wake zao alisema  Ngasa
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa