Na
Walter Mguluchuma
Katavi
Katika hari
isiyotarajiwa baadhi ya Wanafunzi Wasichana wa shule ya Sekondari ya
Mpanda Ndogo Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi wamekutwa wakiwa kwenye bweni
lao walilokuwa wamelala huku wakiwa wamepoteza fahamu na miili yao
kuchanjwa chale bila wao kujitambua
Tukio hilo
la ajabu lilitokea usiku wa kuamkia jana shule hapo tukio ambalo
limethibitishwa kutokea na Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Paza Mwamlima
Kwa mujibu wa
Mwenyekiti wa Bodi ya shule hiyo iliyoko umbali wa kilometa 18 kutoka Mji
wa Pascal Mnyongi alisema kuwa bweni hilo la
wasichana lilikuwa na jumla ya wanafunzi 40 ambao walikuwa wamelala kwenye
bweni hilo
Alisema
siku hiyo kabla ya tukio hilo wanafunzi hao wasichana walikwenda
kujisomea darasani kama ambavyo ilivyokuwa kawaida yao na walijisomea hadi
majira ya saa nne usiku na kisha walirudi kwenye bweni lao na kulala
Alieleza
ilipotimia jana majira ya saa kumi na mbili na nusu asubuhi mwanafunzi
mmoja wa kidato cha tatu aitwaye Terezia Joseph aliamka na
kwenda shule kwa lengo la kuwahi kupiga namba kwa ajiri ya kuhesabiwa kwa
wanafunzi waliowahi kufika shuleni hapo huku akiwa amewaacha wenzake
wakiwa wamelala
Mwenyekiti
wa Bodi hiyo ya shule alieleza Waalimu wa shule hiyo walishitushwa kuona
muda unazidi kwenda huku wanafunzi waliokuwa wakilala kwenye bweni hilo wakiwa
hawaonekani
Waalimu
hao waliamua kwenda kwenye bweni hilo ilikujua kilichokuwa kimewafanya
wanafunzi hao washindwe kuwepo shuleni mida hiyo wakati sio kawaida yao
Alisema
waalimu hao walipofika kwenye bweni walijaribu kuwaita kwa kuwaamsha wanafunzi hao
lakini hawakuweza kuitikia hari ambayo ilizidikuwashitua waalimu wao na kuamua
kusukuma kwa nguvu mlango wa kuingilia ndani lakini walishindwa kufungua
Ndipo
walipomwita mwanafunzi mwenza Terezia Joseph ajaribu
kuufungua mlango huo ambao ulikuwa umewashinda waalimu wake
Alieleza
ndipo Terezia alipofika hapo na aliposukuma mlango huo ulifunguka
na kisha waalimu waliingia ndani ya bweni hilo na kuwakuta wanafunzi hao
wasichana wakiwa wanagalala chini ya vitanda vyao huku wakiwa hawana fahamu na
huku sehemu zote za miili yao ikiwa imechanjwa chale na mtu asiyefahamika
Alisema
kati yao wanafunzi 12 hari zao zilikuwa ni mbaya hari ambayo
iliwalazimu kuwapeleka kwenye zahanati ya Jijiji cha Ifukutwa na baada ya
kupatiwa matibabu hali zao ziliendelea vizuri na wameisha ruhusiwa kurudi
nyumbani kwao
Mnyogi
alisema baada ya kutokea kwa tukio hilo bodi ya shule ilifanya kikao cha
dharula na wazazi wa wanafunzi wanaosoma shuleni hapo na Mwenyekiti wa Waganga
wa jadi wa Kata hiyo ya Mpanda Ndogo kujadili hali hiyo ambayo
imekuwa ikitokea mara kwa mara
Alisema
Mwenyekiti wa Waganga wa Jadi aliwaeleza kuwa kazi hiyo
ya kuzuia matukio hayo yasiendelee anaweza kuifanya na kuondoa tatizo
hilo kabisa shuleni hapo ila wanatakiwa wamlipe wazazi gharama kidogo ndipo
wazazi wa wanafunzi walipochangishana na kufikisha kiasi cha shilingi Tsh
70,000 na kumkabidhi
Alieleza
mwezi januari mwaka huu kulitpkea matukio mawili kwenye bweni hilo
ambapo tukio la kwanza nguo zao za ndani zilikutwa zimepangwa
chini kulingana na idadi ya wanafunzi wanaolala humo na tukio la pili wanafunzi
hao walijikuta wakiwa wamefanya mapenzi bila wao kujitambua
Kwa upande wake
Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Paza Mwamlima amethibitisha kupokea kwa
taarifa za tukio hilo la kushangaza
Amesema
amesema anatarajia leo kufika shuleni hapo na kufanya kikao na bodi ya
shule , wazee maarufu ,na waganga wa jadi na viongozi wa madhehebu ya Dini
mbalimbali kujadili hari hiyo
MWISHO
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
0 comments:
Post a Comment