Na Walter
Mguluchuma
Katavi
Baraza la
Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi wamepirisha pendekezo la kuhamishia makao yao makuu kutoka yaliko sasa Mpanda Mjini
na kuhamia katika eneo la Kijiji
cha Majalila Kata ya Ntongwe Wilayani hapa
uamuzi huo
ulipitishwa jana kwenye kikao
cha baraza maalumu la madiwani
wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda kilichofanyika kwenye ukumbi wa Idara ya
maji mjini hapa kikao hicho ambacho
kiliongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Yassin Kiberiti kilichouzuriwa
pia na Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dr Ibrahimu Msengi
Halmashauri hiyo
iliagizwa na Wizara ya TAMISEMI ihamishe makao yao
yaliposasa mjini Mpanda na kuhamia
kwenye maeneo yao iliwawe karibu
na wananchi wao
Awali
Baraza hilo la madiwani walikuwa
wamapendekeza kuhamishia makao yao makuu
katika Tarafa ya Kabungu eneo
ambalo lilikataliwa kutokana na sehemu hiyo kuwa karibu na Mji wa Mpanda
Katika kikao hicho cha Baraza la madiwani zilitolewa taarifa mbili za timu ya wataalamu ambapo moja iliteuliwa na Katibu Tawala wa Mkoa na nyingine iliteuliwa
na Halmashauri hiyo ilikuangalia vigezo vilivyo kuwa vimetolewa na TAMISEMI kuhusiana
na sifa za mahari panapositahili kuwa
makao makuu ya Halmashauri
Mapendekezo hayo ya timu hizo za
wataalamu zilitofautiana wakati ile timu ya wataalamu walioteuliwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa
Katavi walipendekeza makao hayo yahamia
katika katika eneo la Kamikusu kata ya Katuma umbali wa Kilometa 65 kutoka Mpanda Mjini wakati timu ya
wataalamu wa Halmashauri walipendekeza
makao yao makuu yawe katika Kijiji cha
Majalila Kata ya Ntongwe umbali wa
kilimeta 23 kutoka Mpanda Mjini
Diwani wa kwanza
kuchangia hoja alikuwa ni Diwani wa Kata ya Kabungu Nassor Kasonso ambae alipendekeza kuwa makao makuu ya
Halmashauri hiyo yahamie Kata ya Ntongwe na sio kata ya Katuma kwa kile alichoeleza kuwa eneo hilo linazohuduma muhimu za kibanadamu kuliko Katuma
Pia eneo hilo lipokaribu na barabara kuu inayoelekea Mkoani Kigoma na eneo hilo lipo
kwenye mpango wa kupatiwa umeme wa vijijini wa REA na pia nikatikati
Diwani wa Kata ya Mpanda Ndogo Hamad Mapengo aliliambia Baraza hilo
kuwa kitendo cha kuhamishia makao
makuu kata ya Katuma kutaigharimu Halmashauri hiyo fedha nyingi kwa vile ardhi
ya maeneo hayo yanamilikiwa kihalali na wananchi hivyo watalazimika Halmashauri kuwalipa fidia watu hao kwa ajiri ya ardhi yao
Pia alisema
eneo hilo ni sawa na kujenga
Makao yao makuu porini kwani upo uwezekano wa wananchi kutosogea kujenga makazi yao karibu na makao makuu ya Halmashauri
Kwa upande wake
Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dr Ibrahimu Msengi alisema lengo la msingi kwa Halmashauri hiyo ni kuhama mjini
na kuhamia kwenye eneo lao ili wawe karibu na wananchi wao kuliko ilivyo sasa
Alieleza mapendekezo hayo walioyatowa yatajadiliwa kwenye vikao vya juu na kabla ya
kutolewa maamuzi ni lazima timu ya wataalamu
mbalimbali ifike kwenye maeneo hayo
MWISHO
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
0 comments:
Post a Comment