Na
Walter Mguluchuma
Katavi
Mkuu
wa Mkoa wa Katavi Dr Ibrahimu Msengi amewaeleza wenye Kampuni za ukandasi
wanaofanya shughuli zao kati Mkoa huu kuwa atahakikisha anathibiti
kila kitakachokuwa ninaendelea kwenye ujenzi wa miradi
ya maendeleo ili aweze kubaini thamani ya gharama ya ujenzi
wa miradi kama inalingana na thamani ya fedha
Kauli
hiyo aliitowa hapo jana wakati alipokuwa akizungumza na wakandasi mbalimbali wa
Mkoa wa Katavi pamoja na wataalamu wa Halmashauri zote za Mkoa wa Katavi
kwenye ukumbi wa Idara ya Maji Mjini hapa
Alisema
Mkoa wa Katavi umekuwa na tatizo la miradi mingi ya ujenzi kujengwa chini ya
kiwango kisicholidhisha kutoka na wataalamu kutowakagua kazi zao kwa wakati
Inashangaza
kuona majengo yaliyojengwa mwaka 1971 yakiwa yamejengwa kwa kiwango kizuri
wakati huo kulikuwa na zana duni za ujenzi lakini leo hii
kuna zana bora za ujenzi na makampuni mengi ya Wakandasi majengo
yamekuwa yanajengwa ovyo
Alisema
kuanzia sasa mkandasi yoyote atakae pewa kazi ya kujenga jengo la Serikali
katika Mkoa wa Katavi ahakikishe anakuwa na mafundi wenye utaalamu
wa kujenga vinginevyo wakijenga ovyo watalazimika kuridia
kujenga kwa gharama zao wenyewe na hawata lipwa
Alifafanua
ujenzi wa majengo kujengwa chini ya kiwango umekuwa ukisababishwa na wakandasi
na wataalamu wa Halmashauri kutotimiza wajibu wao wa kuwajibika
kuwasimamia wakandarasi
Alisema
mkandarasi yoyote ambae anaona hawezi kujenga miradi kwa
kiwango kinachositahili atanyimwa tenda ya kufanya kazi
na ni bora akatafute sehemu nyingine ya kufanyia kazi
Vilele
kwa wataalamu ambao wataonekana wakuwa wameshindwa kutimiza wajibu wao
watachukuliwa hatua za kinidhamu za kiutumishi
Dr
Msengi alikataa sababu zinazowafanya wakarasi wachelewe kukamilisha
miradi na kujenga chini ya kiwango zilizotolewa kwenye kikao hicho na
mwakilishi wao Nashon Petro ambae alidai kuwa kiwango cha fedha za
ujenzi huwa zinakuwa ni ndogo na gharama ya vifaa vya jenzi ziko
juu kutokana na mazingira ya huku hasa wakati wa masika
Sababu
nyingine ni kucheleweshewa malipo yao kwa muda unaositahili kutokana na
kuchelewa kukaguliwa shughuli zao na wataalamu wa Halmashauri
Madai hayo yalipingwa na Rc kwa kile alichoeleza kuwa endapo fedha
zingekuwa ni ndogo wasingekuwa wanachukua tenda ya ujenzi kwani
gharama hiyo huwa wanakuwa wanaifahamu kabla ya ujenzi
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
0 comments:
Post a Comment