Home » » Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dr Ibrahimu Msengi amewaagiza watu wote waliovamia kwenye maeneo ya vyanzo vya maji na hifadhi za mistu na kingo za mito waondoke kwa hiari

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dr Ibrahimu Msengi amewaagiza watu wote waliovamia kwenye maeneo ya vyanzo vya maji na hifadhi za mistu na kingo za mito waondoke kwa hiari


Na  Walter  Mguluchuma
Katavi  yetu blog
Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dr  Ibrahimu  Msengi   amewaagiza watu wote waliovamia  kwenye maeneo  ya vyanzo vya maji na hifadhi za mistu na kingo za mito  waondoke kwa hiari kabla ya Serikali haija  waondoa kwa nguvu kwenye maeneo hayo
Rc Dr  Msengi  alitowaagizo hilo hapo jana  kwenye   siku ya upandaji miti  kimkoa wa Katavi iliofanyika  kimkoa kwenye Tarafa ya Mwese Wilaya ya Mpanda  wakati alipokuwa akiwatutubia Wananchi
Alisema  hari ya  hari ya  uharibifu wa mazingira katika Mkoa wa Katavi  imekuwa ikiongezeka siku hadi siku  huku  wananchi na viongozi wa maeneo hayo  wakiwawanaona kama ni jambo la kawaida
 Alieleza  kuwa kila mtu anahaki na wajibu  wa kuhakikisha anatunza mazingira  na Sesrikali ya Mkoa wa Katavi  haita kuwa  na huruma  kwa mtu yoyote  ambae   atakae patikana  anaharibu  mazingira hivyo watu wote wanaoishi kwenye vyanzo vya maji  na hifadhi za mistu na kwenye kingo za mito waanze kuondoka kwa hiari kabla ya Serikali haija waondoa kwa nguvu kwani jambo la kuwaondoa halitakuwa na mjadala tena
 Alifafanua   wapo  baadhi ya watendaji wa vijiji na Kata wamekuwa wakiwaonea watu aibu  na kuwaogopa  na kuwaacha  wakiangusha miti ovyo  bila utaratibu  huku  viongozi  hao wakiwepo kwenye maeneo hayo
 Alisema kuanzia sasa  mtendaji wa Kijiji na Kata ambae  kutatokea uharibifu wa mazingira kwenye eneo lake  atawajibishwa  yeye  kwa kushindwa kutekeleza wajibu wake
 RC Msengi alisema   hari ya  uharibifu wa mazibgira  imekuwa ni  kubwa sana  katika Mkoa wa Katavi na tayari hari hiyo imeanza kusababisha upungufu wa mvua katika Mkoa huu kwani mvua zinazonyesha kwa sasa hazilingani na mvua zilizokuwa zikinyesha miaka ya nyuma kabla ya mazingira  yalipo  kuwa hajaharibiwa na watu
 Alisema  wakulima na wafugaji  waitwe na  waelezwe na viongozi wa kwenye maeneo yao  sheria za utunzaji wa  mazingira zilivyo  ili Serikali inapowachukulia hatua wasione kuwa wameonewa
Alifafanua kuwa lengo la Serikali ya Mkoa wa Katavi sio kuwafukuza wafugaji na wakulima  bali ni kuhakikisha mzingira yanatunzwa vizuri na watu hawakati miti ovyo
 Alisema Halmashauri za Mkoa wa  zote zilizopo  katika  Mkoa wa Katavi  zianze  kuangalia  utaribu  wa namna  ya kuzuia  watu wasikate miti ovyo  na  kila mti unaokatwa uwe unajulikana unakatwa kwanini na kwa matumizi yapi
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya  Wilaya ya Mpanda Estomiel  Chang’ah alisema zoezi la kuwahamisha watu wanaoishi kwenye vyanzo vya maji na hifadhi za mistu na kuharibu mazingira limekuwa likikwamishwa na viongozi wa siasa
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa