Home » » WATU WAWILI WAKAMATWA NA MENO YA TEMBO YA THAMANI YA TSH MILIONI 157

WATU WAWILI WAKAMATWA NA MENO YA TEMBO YA THAMANI YA TSH MILIONI 157



Na   Walter  Mguluchuma
Katavi
Jeshi la Polisi  Mkoani  Katavi limewakamata na  linawashikilia watu wawili kwa tuhuma za kuwakamata na meno  ya Tembo  vipande 22 yenye uzito  wa kilogramu 46 yenye thamani ya shilingi milioni  157,500,000 sawa  na Tembo saba waliouwawa  wakati wakiwa wanataka  kuyasafirisha kwenye  basi kutoka Mpanda kuyapeleka Mkoa wa Kigoma
Kaimu Kamanda wa  wa  Jeshi la Polisi wa Mkoa wa Katavi   Rashid Mohamed aliwataja watuhumiwa hao  waliokamatwa kuwa ni  Justine  Baluti (Zolros)(39) Mkazi wa Kijiji cha  Ivungwe makazi ya Wakimbizi ya Katumba Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi  na  Bobifaphace  Hoza (40) Mkai wa  Kalele  Wilaya ya Kasulu Mkoa  wa Kigoma
  Alisema watuhumiwa hao wote  wawili walikamatwa hapo jana majira ya saa  kumi na mbili asubuhi katika eneo la stendi ya mabasi ya Mpanda iliyoko katika mtaa wa Mji wa Zamani  mjini  Mpanda
  Siku hiyo ya tukio  majira hayo ya saa kumi na mbili asubuhi  Askari  Polisi walikuwa dolia kwenye  eneo la stendi ya mabasi ya Mpanda yaendao Mikoani walimtilia shaka  mtuhumiwa Justine Baluti  aliyekuwa anapakia mizigo yake kwenye basi la Kampuni ya Adventure lenye Namba za usajiri  T.992 BUT  aina ya Nissani  lililokuwa likielekea Mkoani Kigoma
 Kaimu Kamanda   Rashid  Mohamed  alieleza  baada ya polisi kumtilia mashaka mtuhumiwa huyo  na yeye alipowaona polisi kwenye  eneo hilo alitaka  kutoroka kwenye eneo hilo  hata hivyo polisi walifanikiwa kumweka chini ya ulinzi
 Polisi baada ya kupekua mizigo  ya mtuhumiwa  Justine  walimkuta  akiwa na meno  ya Tembo  vipande 15  yenye uzito wa kilogramu 33  vyenye thamani ya Tshilingi milioni  90 sawa na Tembo  wanne waliouwawa   yakiwa  ameyahifadhi ndani ya  mabegi makubwa mawili
 Alisema  baada ya  Justine kupekuliwa na kukutwa na meno hayo ya Tembo  mtu mwingine ambae  inaonesha  alikuwa na mtuhumiwa  alitupa beji lake la rangi ya ugoro na kisha kutokomea  kusiko julikana
Polisi  waliweza kulikamata Basi hilo la Kampuni  ya Adventure na kulipeleka hadi kituo cha Polisi cha Wilaya ya Mpanda kwa ajiri ya upekuzi zaidi
 Kaimu Kamanda Rashid  alisema baada ya polisi kufanya  ukaguzi wa kina  kwenye basi hilo walifanikiwa  kumkamata mtuhumiwa  Bonifaphace   Hoza  akiwa na beji moja  alilokuwa amelihifadhi  chini  chini ya  siti  Namba K.3 Lililokuwa  ndani yake na vipande  saba  vya meno ya Tembo  yenye uzito wa kilogramu  13 yenye thamani ya Tsh milioni 67,500,000 ambayo ni sawa na tembo  watatu waliouwawa
 Alisema  watuhumiwa hao wawili  wanaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi  kwa uchunguzi zaidi  na watafikishwa mahakamani mara baada ya upelelezi kukamilika ili wajibu tuhuma  zinazowakabili
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa