Home » » HOT NEWS: MHUDUMU WA AFYA JELA MIAKA MITATU KWA KUPOKEA RUSHWA YA TSH 25,000

HOT NEWS: MHUDUMU WA AFYA JELA MIAKA MITATU KWA KUPOKEA RUSHWA YA TSH 25,000



Jiunge na Huduma ya Tone Mobile News Bure kabisa kupitia Whatsapp yako na uwe wa kwanza kupata kile kinachotokea ni Rahisi sana Ingia katika uwanja wa kuandika ujumbe mfupi wa maneno katika Whatsapp yako kisha andika TONE MOBILE NEWS tuma kwenye namba 0756364660 utapokea ujumbe kuwa umeunganishwa.


Na  Walter  Mguluchuma 
Mpanda  Katavi
Mahakama ya Wilaya ya Mpanda  imemuhukumu  mhudumu wa Afya wa Hospitali ya Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi  Peter  Nyirenda  kifungo cha miaka mitatu  jela baada ya kupatikana na hatia  ya  kosa  la  kuomba  na  kupokea Rushwa ya Tsh 25,000
Hukumu  hiyo ilitolewa na Hakimu  Mkazi  Mfawidhi  wa Mahakama ya Wilaya ya Mpanda Chiganga Ntengwa  baada ya mahakama kulidhika  na ushahidi  uliotolewa  mahakamani  hapo na upande wa mashitaka na utetezi
 Awali katika kesi hiyo  mwendesha mashitaka wa TAKUKURU  Bahati  Haule  aliileza mahakama kuwa  mshitakiwa alitenda kosa hilo  hapo  julai  15 mwaka huu  katika Hospitali ya Wilaya ya Mpanda
Alidai kuwa siku hiyo ya tukio  mshitakiwa akiwa  mhudumu wa Afya  katika wodi  ya watoto katika Hospitali ya Wilaya ya Mpanda  aliomba na kupokea  kutoka kwa msiri  iliaweze  kumpatia  matibabu mtoto wake  aliyekuwaamelazwa  katika wodi ya watoto  katika Hospitali ya Wilaya ya Mpanda
Mwendesha mashitaka Haule alieleza  baada ya taarifa  kufikishwa TAKUKURU  waliandaa mtego na kufanikiwa  kumkamata mtuhumiwa   siku hiyo ya tarehe 15 Julai mwaka huu
 Mwendesha mashitaka wa TAKUKURU alimsomea mshitakiwa  mawili ambayo ni kuomba Rushwa ya Tsh 25,000 na kupokea Rushwa  ya Tsh 25,000 kinyume na matakwa ya mwajiri wake  kinyume na kifungu cha sheria  cha 15 (1)(a) cha sheria ya kuzuia na kupambana na Rushwa  namba 11 ya mwaka 2007
Mshitakiwa  Peter Nyirenda  baada ya kusomewa mashataka hayo mbele ya Hakimu Chiganga Ntengwa alikiri mahakamani kutenda kosa hilo  la kuomba na kupokea Rushwa
 Hakimu mkazi  Chiganga Ntengwa aimtaka mshitakiwa  kabla ya kutolewa kwa hukumu  kama anayosababu yoyote ya msingi ya kuiomba mahakama impunguzie adhabu aieleze mahakama  ambapo mshitakiwa aliomba mahakama isimpe adhabu kwa kuwa ndio kosa lake la kwanza kufikishwa mahakamani
Mwendesha mashitaka wa TAKUKURU   Bahati  Haule alipinga vikali utetezi huo  kwa kile alidai kuwa  kumekuwepo na malalamiko mengi  ya kuhusiana na Rushwa  kutoka Idara ya afya  katika Hospitali ya Wilaya ya Mpanda  na  yanaathari kubwa  kwa jamii kwani hugharimu  uhai na  afya ya mgonjwa
HakimuChiganga  akisoma hukumu hiyo alisema  mtuhumiwa  baada ya kupatikana na hatia hiyo mahakama inamuhukumu kwenda jela miaka mitatu au kulipa faini ya shilingi Tsh 500,000   hata hivyo mtuhumiwa aliweza kulipa faini hiyo na kunusulika kwenda jela
Pia hakimu  Chiganga aliiambia  mahakama kuwa hakuna kumbukumbu  zozote  ambazo zinaonyesha mshitakiwa kuwahi kutenda kosa hilo na mshitakiwa  katika kesi hiyo  hakuweza  kuisumbua  wala kuipotezea muda  mahakama  kwa kitendo chake cha kukiri kosa

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa