Home » » DC MADIWNI WA NSIMBO: TAMBUENI MNAO WAJIBU WA KUSIMAMIA MIRADI YA MAENDELEO KWENYE MAENEO YENU‏

DC MADIWNI WA NSIMBO: TAMBUENI MNAO WAJIBU WA KUSIMAMIA MIRADI YA MAENDELEO KWENYE MAENEO YENU‏



Jiunge na Huduma ya Tone Mobile News Bure kabisa kupitia Whatsapp yako na uwe wa kwanza kupata kile kinachotokea ni Rahisi sana Ingia katika uwanja wa kuandika ujumbe mfupi wa maneno katika Whatsapp yako kisha andika TONE MOBILE NEWS tuma kwenye namba 0756364660 utapokea ujumbe kuwa umeunganishwa. 

Na    Walter Mguluchuma
Mpanda Katavi
Mkuu wa  Wilaya  ya  Mlele Mkoa wa  Katavi   Kanali  Ngemela  Lubinga  amewataka Madiwani wa Halmashuri ya  Nsimbo  kuhakikisha  wanatambua  kuwa wanao wajibu wa kusimamia miradi yote ya maendeleo ilipo kwenye maeneo yao
Wito huo kwa madiwani aliutowa  hapo juzi wakatiakifungua mkutano Mkuu wa mwaka  wa  Baraza la  Madiwani  wa  Halmashauri ya  Nsimbo uliofanyika kwenye ukumbi  wa Halmashauri  hiyo
Kanali  Lubinga  alisema Madiwani wamekuwa wakitambua kuwa jukumu la kusimamia  miradi ya maendeleo kwenye maeneo yao  sio jukumu lao  na badala yake wamekuwa wakiwaachia watendaji wao ndio wasimamie peke yao
Alifafanua  miradi mingi imekuwa haiendi  vizuri  kwenye maeneo yao  hivyo wanao wajibu wa kuwasaidia  kusimia  watendaji wao  shuguli za maendeleo zilizopo kwenyw  Kata zao  na kazi ya Diwani  ni kuwasimamia  watendaji   sio kuwakataa watendaji wao
Alisema Diwani yoyote  ambae  hatimizi wajibu wa majukumu   wala hajuwi wajibu wake huyo sio  Diwani  na madiwani wa namna hiyo hawanafaida kwa wananchi na kwa Halmashauri
Lubinga aliwaeleza  Halmashauri hiyo imebahatika kuwa na  rasilimali nyingi ambazo  wamekuwa  hawazitumii vizuri kwa faida ya  Halmashauri ya  Nsimba 
Alisema yako makampuni yanayochimba madini  na  makampuni ya   wawindaji wa wanyama   Halmashauri inapaswa  iandae  uratibu kwa ajiri ya  makampuni  haya kabla ya kuanza kufanya  shughuli  kwenye  Halmashauri hiyo  lazima makampuni hayo yawe yanachangia kwanza kwenye maswala ya elimu na  afya
Alieleza  niabu kwa Halmashauri hiyo  kuona zipo baadhi ya  shule za msingi wako wanafunzi wanasoma huku wakiwa wanakaa   chini na badhi ya  shule za  Sekondari  zimeshindwa kukamilisha ujenzi wa  majengo ya maabara wakati na makampuni hayo yapo  hakikisheni  Halmashauri mnaweka utaratibu kwa makampuni kuchangia
Kwaupande wake  Mwenekiti wa Halmshauri ya  Nsimbo  Medi   Asenga  alisema madiwani watahakikisha  maelekezo hayo yaliotolewa watayatekeleza 
Alisema  Halmashauri  hiyo kuanzia  saasa  itaakikisha  shughuli zote za miradi ya maendeleo wanapewa  makandarasi wenye uwezo  na madiwani wataisimamia miradi hiyo kwa karibu kwa kushilikiana na watendaji wao
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa