Home » » MTOTO AFA BAADA YA KUTUMBUKIA NDANI YA NDOO YA MAJI‏

MTOTO AFA BAADA YA KUTUMBUKIA NDANI YA NDOO YA MAJI‏

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Na   Walter  Mguluchuma
Mpanda Katavi
Mtoto mmoja   aitwaye  Paulina  David  3   Mkazi  wa Kijiji  cha  Sungamila  Kata  ya Kasokola   Wilaya  ya Mlele  Mkoa  wa Katavi  amefariki  Dunia  baada  ya kutumbukia  ndani ya ndoo ya maji  akiwa  nyumbani  kwao
Tukio  la  kifo  cha mtoto huyo  lilitokea  hapo juzi  Kijijini  hapo  majira ya saa kumi  jioni  wakati  marehemu  huyo   alipokuwa   nyumbani kwao  alipokuwa  akicheza  na  dada  yake  aitwaye  Stela  David  5 
Siku  hiyo  mama  yake  mzazi na  Marehemu  huyo  aitwaye  Winfrida  Sanane  alimuacha  nyumbani  marehhemu  akiwa  anacheza  na Dada  yake  huyo  na  yeye alielekea  mtoto  kwenda kufua nguo  katika  mto  ulioko  kijijini  hapo
Baada  ya mama  yao kuondoka   marehemu  na dada yake  waliendelea  na  michezo yao  mbalimbali  kwa muda mrefu  aliambayo ilimsababishia  marehemu  apatwe na kiu  cha  maji ya  kunywa
Ndipo  marehemu  alipomweleza  dada yake  kuwa  anajisikia kiu cha maji na Dada yake alimweleza kuwa kwenye ndoo ilipo  nje  karibu na jiko  ndio  ina maji ya kunywa hivyo  akanywe  maji ya kunywa  hapo
Marehemu  baada ya kuelekezwa  mahari maji yalipoalielekea hapo na  ndipo alipoyaona maji yakiwa   yako kwenye ndoo ya plasitiki yakiwa nusu ndoo na ndani yake kulikuwa na  babakuli  ambalo marehemu alipoliona alitaka kulichukua kwa ajiri ya kutekea maji ili anywe
Wakati  anataka kuchukua  bakuli hilo  ndani ya ndoo ya maji  ndio  alipotumbukia kwenye ndoo hiyo kwa kutumbukiza kichwa huku miguu ikiwa juu hari ambayo ilimfanya  dada yake   amkimbilie na kwenda kumtoa ndani ya ndoo
Dada yake huyo  na marehemu baada ya kumtoa mdogo wake na kumlaza chini alishitushwa ha hari aliyokuwa  nayo  na kumfanya akimbie kwenda kwa majirani  kwa ajiri ya kuomba msaada  ambapo majirani walifika kwenye eneo hilo baada ya muda mfupi na kumkuta marehemu akiwa  ameisha fariki Dunia
Kamanda wa Jeshi la Polisi wa Mkoa wa Katavi  Kamishana msaidizi  mwandamizi Dhahiri  Kidavashari  amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na  alisema ndugu wa marehemu  huyo  waliamua kufanya mazishi ya mtoto huyo hapo  jana  baada ya kutokuwa na mashaka yoyote kuhusiana na kifo hicho

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa