Na Walter Mguluchuma
Mpanda Katavi
Wanawake wawili
mama na Mtoto wake wakazi wa
Kijiji cha Mnyagala Tarafa ya Kabungu Wilaya ya Mpanda Mkoa wa
Katavi wamefariki Dunia baada ya kupigwa na Radi na Kufa hapo hapo wakati wakiwa njiani wakiwa wanatokea kwa jirani yao
Kwa mujibu wa
Kamanda wa Jeshi la Polisi wa Mkoa wa
Katavi Kamishina mwandamizi Msaidizi
Dhahiri Kidavashari alisema tukio
hilo lilitokea hapo A
prili 22 mwaka huu majira ya saa kumi na mbili jioni kijijini hapo
Kamanda
Kidavashari aliwataja waliokufa kwa kupigwa
na Radi ni Migu Samwel 46 na
mwanae wakike aitwaye Nsungulwa Kasanzu 15 wote wawili wakiwa wakazi wa kijiji hicho cha Mnyagala
Alisema kabla
ya vifo hivyo vya mama na mwanae marehemu hao
walikuwa wamekwenda kwa jirani
yao kwa lengo la kumsalia na wakati wako
huko waliona wingudogo la mvua
likiwa limetanda hewani
Alieleza
kutokana na kuwepo
kwa wingu hilo dogo la mvua
marehemu hao walimuga jirani
yao kuwa wanawahi kurudinyumbani kwao kabla mvua ya haija anza
kunyesha kwani waliondoka nyumbani huku
baba mwenye nyumba akiwa hayupo
alikuwa amekwenda kwenye shughuli zake za ufundi wa baiskel kijijini hapo katika eneo linaloitwa Center
Alifafanua wakati
wakiwa wanaelekea i walipofika
jirani na nyumba yao umbali wa mita 15 ndipo walipopigwa na radi
na kufa hapo hapo ambapo mama
alipigwa na radi sehemu ya kifuani na
mwanae alipigwa na radi
sehemu ya kichwani
Alisema baada ya
kuwa wamepigwa na Radi
na kufafa hapo hapo miili ya
marehemu hao iliokotwa na majirani
walikuwawakipita kwenye eneo hilo baada ya mvua ndogo ilinyesha kuwa
imekatika
Kidavashari alieleza
majirani hao baada ya hapo walitowa
taarifa kwenye uongozi wa Serikali ya Kijiji ambao
nao walifika kwenye eneo hilo na kisha walitowa taarifa za vifo vya marehamu
hao kwa jeshi la polisi Wilaya
ya Mpanda
Alisema miili ya
marehemu hao ilitarajiwa kuzikwa
jana kijijni hapo mara
baada ya taratibu za kidaktari
zitakapokuwa zimekamilika na
jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi
limetowa wito kwa wakazi wa Mkoa huo
huacha kutembea barabarabi wakati wa
mvua na waepuke kupita kariu
na miti
0 comments:
Post a Comment