Home » » ROLI LAPINDUKA KUMI WAJERUHIWA NA KULAZWA HOSPITALINI‏

ROLI LAPINDUKA KUMI WAJERUHIWA NA KULAZWA HOSPITALINI‏

Na Walter  Mguluchuma-Blogs za Mikoa
Mpanda  Katavi
 Watu kumi wamejeruhiwa na kulazwa katika Hospital ya Wilaya ya Mpanda  baada ya Roli ana ya Fuso walilo  kuwa wakisafiria  kupinduka  baada ya kushindwa kupanda mlima
Ajari hiyo  ilitokea hapo juzi  majira ya saa kumi na mbili asubuhi  huko katika   Kijiji cha Kanoge makazi ya Wakimbizi  ya Katumba Wilaya ya Mlele  Mkoa wa Katavi  ajari ambayo ililihusisha gari lenye namba za usajiri  T 210BBZ  aina ya fuso  lililokuwa likiendeshwa na  Makaliasi Mmanzi  (36) mkazi wa Mtaa wa Makanyagio Mjini Mpanda
Kamanda  wa Polisi wa Mkoa wa Katavi Dhahiri Kidavashari aliwataja majeruhi hao kuwa ni Tano Salumu  (16)  Matheo Mswanya  (27) waliojeruhiwa miguu Juma Maulidi( 41)  alipata majeraha kichwani  Salimu Hamisi (27) alipata maumivu kifuani Abeiry  Silivesto  (20)  aliye humia kifuani wote wakazi wa Mtaa wa Makanyagio Mjini Mpanda
Aliwataja majeruhi  wangine  kuwa  ni Hussein  Mohamed  (32)  mkazi wa Mtaa wa Nsemlwa aliumia mguu  Simon Canshuni  (38)  mkazi wa Mtaa wa Kawajense ambae amevunjika mguu  wa kushoto Frenk  Masatu (15) Ibrahimu Mnyaki (45) aliye umia kiono na miguu wakazi zi wa mtaa wa kawajense  na Mazoe Kasanga  (30) mkazi wa Kijiji cha Kakese  wote wakazi wa Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi
Kamanda Kidavashari alieleza kuwa gari hilo ambalo lilikuwa limebeba watu hao lilikuwa likitokea Mpanda mjini  likielekea katika kijiji cha Ugalla Wilaya ya Mlele  mkoani hapa
Alisema wakati gari hilo lilipo fika  katika eneo la mlima wa Kanoge  lilishindwa kupanda mlima na kuanza kurudi nyuma na kisha liligonga gema  upande wa kulia wa barabara  na kupinduka
Majeruhi  hao wote wamelazwa katika Hospital ya Wilaya ya Mpanda wakipatiwa matibabu na watatu kati yao hari zao ni mbaya
Kamanda Kidavashari  amewataka wamiliki wamiliki wa vyombo vya usafirin kujenga utaratibu wa kufanyia matengenezo  vyombo vyao vya usafiri  na kuzingatia sheria  za usalama barabarani
Alisema dreva wa gari hilo anashikiliwa na polisi na anatarajiwa kufikishwa mahakamani wakati wowote  ili aweze kujibu mashitaka

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa