Home » » WAKAZI WA MJI WA MPANDA KUONDOKANA NA TATIZO LA UHABA WA MAJI

WAKAZI WA MJI WA MPANDA KUONDOKANA NA TATIZO LA UHABA WA MAJI

Na  Walter  Mguluchuma
Mpanda Katavi
Lile tatizo la uhaba wa maji lililokuwa likiwakabili  wakazi wa Mji wa Mpanda  kwa kipindi kirefu sasa  limepatiwa ufumbuzi  na halitakuwepo tena  kuanzia  mwakani mara hapo utakapo kuwa umekamilika mradi wa chanzo cha maji cha Ikorongo kilichopo  katika Makazi ya wakimbizi ya Katumba
Hayo yamesemwa hapo jana na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Mpanda Enock Gwambasa  mara baada  ya ziara yake  ya kukagua  mradi huo wa chanzo cha maji cha Ikorongo
Mradi huo wa maji wa chanzo cha Ikorongo umetokana na msaada uliotolewa na benki ya dunia ambayo ndio itakayogharamia mradi huo ambao ni mkombozi kwa wakazi wa Mpanda na vijiji vinavyozunguka mji huo
Alisema  mradi huo  utakapo kamilika unatarajiwa kugharimu  jumla ya shilingi  biloni  tatu na  milioni miatatu  na utakamilika mwezi june mwakani  na utamaliza tatizo kabisa kwa mji wa Mpanda na vijiji vinavyo zunguka mji huo
Alisema eneo la kujengelea chanzo cha  maji kilichopo Ikolongo kinatajiwa kukamilika katikati ya mwezi huu  chanzo hicho cha maji kinauwezo wa kuzalisha lita milioni mbili na laki mbili kwa siku
Gwambasa alifafanua kuwa  ujenzi wa tanki la kuhifadhi maji  hayo  lenye uwezo wa kuhifadhi lita milioni moja  utakamilika  mwishoni mwa mwezi huu wa oktoba
Alieleza kuwa  mara baada ya shughuli hizo kukamilika  itafuata kazi ya uchimbaji wa  wa mitaro na usambazaji wa bomba  kutoka kwenye chanzo hicho cha Ikolongo hadi mjini Mpanda
Kwa upande wake kaimu Mwandisi wa Maji wa Halmashauri ya Mji wa Mpanda Festo  Katanti  alieleza kuwa mji wa Mpanda  unawakazi  102,360  hivyo  mradi huo utafanya  kuwa na zida ya maji  ambayo yanaweza pia kupelekwa hadi kwenye Tarafa ya Nsimbo  wilaya ya Mlele iliyoko  katika  Halmashauri ya Nsimbo
Alisema  maji ambayo yatakuwa yamezidi kwenye tanki  lililopo  katika Mtaa wa Kazima  watahakikisha maji hayo hayapotei bure  bali  wanaangalia utaratibu wa jinsi yatakavyo tumiwa na wananchi wa jirani na Tanki hilo
Kaimu mhandisi wa maji wa Halmashauri ya mji wa Mpanda bwana Katanti alieleza kuwa mradi huo wa ujenzi wa chanzo cha maji na tenki la maji unafanywa na kampuni iitwayo Pet Cooperation Ltd inayomilikiwa na mkandarasi wa kitanzania

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa