Na Walter
Mguluchuma
Katavi
Mtu Mmoja Ngusa
Solea (32) Mkazi wa Kijiji cha Matandalani Tarafa ya Nsimbo amekutwa amekufa baada ya kunywa pombe ya
kienyeji aina ya Komoni inayosadikiwa kuwa na sumu
Kamanda wa polisi
wa Mkoa wa Katavi Dhahiri Kidavashari
alisema tukio la kifo cha mtu
huyo kilitokea hapo juzi majira ya saa tatu asubuhi
Alisema Ngusa
siku hiyo alikutwa akiwa amefariki
dunia nje ya nyumba iliyo kuwa ikiendelea kujengwa Pagara jirani
na nyumba ya Anisety Matongo huku
mwili wake ukiwa unatokwa na damu puani
Kidavashari alieleza kuwa usuku wa
tukio hilo marehemu alionekana
akinywa pombe ya kienyeji aina komoni
nyumbani kwa Anisety Matondo mpaka usiku wa manane
Marehemu hata hivyo
haikufahamika aliondoka saa ngapi
hapo alipo kuwa akinywa pombe na
ndipo siku iliyo fuata majira ya saa tatu asubuhi alipo kutwa kwenye pagara akiwa ameisha kufa
Kamanda wa polisi
wa Mkoa wa Katavi alisema chanzo cha
kifo hicho kinadhaniwa
kuwa ni marehemu alikunywa alikunywa pombe ambayo ilikuwa na sumu
Alieleza mpaka
sasa hakuna mtu au watu waliokamatwa kuhusiana na tukio
hilo na jitihada za kubaini chanzo cha
kifo na upelelezi wa tukio hilo bado
unaendelea
Alisema jitihada za
kumtafuta Anisety Matondo aliko
kuwa akinywa pombe marehemu zinaendelea kwani
Anisety alitoka kijijini
hapo mara baada ya kugundua kuwa marehemu
Ngusa amefariki
0 comments:
Post a Comment