Na Walter Mguluchuma
Mpanda
Mtu mmoja Mkazi wa
kijiji cha Kasekese Tarafa ya
Mwese wilaya ya Mpanda mkoa wa
Katavi Anton David ( 45)
ameuwawa kwa kupigwa na kitu kizito kichwani na watu wasiojulikana
Kamanda wa polisi wa Mkoa wa Katavi Dhahiri
Kidavashari alisema tukio hilo lilitokea
hapo jana majira ya saa nne usiku nyumbani kwa marehemu huyo
Alisema marehemu
alikutwa ndani ya chumba chake muda huo wa saa nne usiku akiwa ameisha kufa huku mwili wake ukiwa umelala kitandani
Baada ya majirani kuuchunguza mwili wa marehemu
walimkuta akiwa na majeraha makubwa
kichwani yaliyo tokana na kupigwa na
kitu kizito sehemu ya kichwa chake
Kamanda Kidavashari ameeleza kuwa jeshi la polisi mkoa wa
Katavi linamshikiia mtu mmoja aitwaye John Mwanandota (35) mkazi wa kijiji hicho cha Kasekese
kuhusiana na tukio hilo
Jeshi la polisi
mkoa wa Katavi limetowa wito
kwa wananchi waendelee
kushirikiana na jeshi la
polisi katika kupambana na uharifu
katika maeneo yao kwa
kuimarisha mfumo wa ulinzi shirikishi na ulinzi
jirani ili kuweza
kuwabaini na kuwakamata watu
wanaotenda uharifu katika
maeneo yao ili waweze kufikishwa
kwenye vyombo vya sheria .
0 comments:
Post a Comment