Na walter MguluchumaMpandaMkazi wa kijiji cha Bulembo makazi ya wakimbizi ya Katumbawilayani Mlele Mkoa wa Katavi Sindebula Msagi (32) amefikishwakizimbani katika mahakama ya hakimu mkazi ya wilaya ya Mpandakwa tuhuma za kumbaka na kumlawiti mwanamke mwenye umri wamiaka 90Mwendesha mashitaka wa jeshi la polisi Ally Mbwijo aliiambiamahakama hiyo hapo juzi mbele ya hakimu mkazi mfawidhi wamahakama hiyo Chiganga Tengwe kuwa mshitakiwa alitenda kosahilo hapo desemba 22 mwaka jana majira ya saa 8 usiku nyumbanikwa kikongewe huyo.Alisema siku hiyo ya tukio mshitakiwa Sindebula alifikanyumbani kwa mama huyo na kuvunja mlango na kisha aliingiandani ya nyumba ya mama huyo ambae alikuwa ni mgonjwa wa kupoozamguu wa kulia na mkono wa kulia kisha alimbaka na kumlawitikwa nguvu mama huyoPamoja na mama huyo kumsihi mshitakiwa asimfanyie kitendo hichoalimweleza kuwa umri wake ni mkubwa hasitahili kufanyiwa hivyolakini mshitakiwa hakujali ombi la mama huyo bali aliendeleakumfanyia unyama kikongewe huyo licha ya kupiga mayowe ya kuombamsaada kwa majirani hakuweza kufanikiwa kutokana na nyumba aliyokuwa akiishi kuwa mbali na majiraniMwendesha mashitaka aliendelea kuiambia mahakama hiyo ambayoililazimika kwenda kusikilizia kesi kwenye eneo la tukiokutokana na hari ya mama huyo kuwa katika hari mbaya yakiafya kuwa mshitakiwa aliendelea kumfanyia unyama mama huyompaka usingizi ukampata na kisha kulala ndani ya chumba cha mamahuyoAlieleza ilipofikia majira ya saa 12 asubuhi ndipo mama huyo alipoweza kufungua dirisha na aliweza kumwona mtu mmoja aitwaye AshabolaElly aliye kuwa akipita jirani ya nyumba yake ndipo alimwonyeshaishara ya kumwita kwa kutumia vidole ili aweze kufika kumpatia msaadaMwendesha mashtaka alisema baada ya Ashobola kuingia ndani alimkutamshtakiwa akiwa amelala chini na ndipo alipoweza kumtambua ilahakuweza kumuamusha kutokana na tabia yake ya ukorofi hivyoilimlazimu akimbie kwenda kutoa taarifa kwa majirani .Majirani waliweza kufika katika eneo hilo huku wakiwa na viongozi wakijiji hicho hata hivyo walikuta mshtakiwa amekwisha amka nakutokomea.Alisema polisi walifanikiwa kumkamata mshtakiwa muda mfupi baada yakuwa ametoka kwenye nyumba hiyo na katika maelezo yake ya awalaimshtakiwa alikiri kutenda kosa hilo kutokana na kile alichodaikilisababishwa na pombe nyingi ya kienyeji aliyokuwa amekunywa aina yaKayogaTaarifa ya daktari aliyemfanyia uchunguzi mama huyo imeonyeshakuharibiwa vibaya sehemu zake za siri na haja kubwa , katika kesi hiyoupande wa mashtaka una mashahidi wanne na mshtakiwa hana shahidiyoyote.Hakimu Mkazi Mfawidhi Chiganga aliamuru mshtakiwa kwenda Rumande hadihapo March 28 mwaka huu kesi yake itakapaosikilizwa.
Home »
» KIJANA WA MIAKA 32 KIZIMBANI KWA KUMBAKA NA KUMRAWITI KIKONGWE WA MIAKA 90
0 comments:
Post a Comment