Home » » AMATI ZA USHAURI WA KISHERIA ZAZINDULIWA KATAVI, WANANCHI WAPATIWA HUDUMA ZA SHERIA BILA MALIPO

AMATI ZA USHAURI WA KISHERIA ZAZINDULIWA KATAVI, WANANCHI WAPATIWA HUDUMA ZA SHERIA BILA MALIPO

Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Katavi, imezindua Kamati ya Ushauri wa Kisheria ngazi ya Mkoa na Wilaya katika Mkoa wa Katavi. 

Uzinduzi huo umefanyika tarehe 8 Septemba, 2026 na kufuatiwa na kliniki ya Sheria bila malipo iliyoanza tarehe 7 Septemba, 2026 katika Viwanja vya Azimio Mpanda Uzinduzi wa Kamati za Ushauri wa Kisheria na Kliniki ya Kisheria bila malipo, ni dhamira ya dhati ya Serikali kupitia Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya kutatua migogoro, kutoa ushauri wa Kisheria kwa wananchi na elimu ya Kisheria bila malipo. 

 Akizungumza katika hotuba yake ya Uzinduzi, Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Mhe. Jamila Yusuph, ameeleza kuwa jukumu la kutatua migogoro katika maisha ya watanzania sio la Serikali pekee ni jukumu la wadau wote wa maendeleo. 

 Mhe. Mkuu wa Wilaya amekuwa mgeni rasmi akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe. Mwanamvua Hoza Mrindoko katika Uzinduzi wa Kamati za Kudumu za Ushauri wa Kisheria ngazi ya Mkoa na Wilaya zimezinduliwa mkoani Katavi, tarehe 8 Septemba , 2026, katika Viwanja vya Azimio, Mpanda.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa