Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi Damas
Nyanda akitowa maelezo kwa Wandishi wa Habari jana ofisini
kwake jinsi jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi lilivyofanikiwa kukamata
silaha tano za kivita aina ya SMG na risasi 15 za SAR na
Bunduki mbili aina ya Gobore katika kipindi cha miezi mitatu
kuanzia Septemba hadi Novemba Silaha hizo na risasi
zilikamatwa katika Wilaya za Mlele na Mpanda .
Silaha za kivita
aina ya SMG na risasi 15 za bunduki aina ya SAR pamoja na
Gobore mbili ambazo zimekamatwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa
Katavi katika kipindi cha miezi mitatu ya kuanzia Septemba hadi
Novemba mwaka huu .
Picha na Walter Mguluchuma/Katavi yetu Blog
Na Walter Mguluchuma/
JESHI la Polisi mkoani Katavi imekamata bunduki risasi ita zikiwemo
SMG nne na risasi 15 za SAR.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi Damas Nyanda alisema
silaha hizo zilikamatwa katika msako maalumu uliofanyika katika
wilaya za Mlele na Mpanda mkoani huo katika kipindi cha Septemba na
Oktoba
Alisema alisema Septemba 02, katika kijiji cha Kalovya , Tarafa
ya Inyonga katika wilaya ya Mlele watu wawili ambao majina yao
yamehifadhiwa walikamatwa wakiwa wanamiliki bunduki aina ya SMG
isiyokuwa na namba kinyume cha sheria .
“Isitoshe Septemba 28 , saa mbili usiku lilifanikiwa mtu
anayeishi katika makazi ya Wakimbi ya Katumba wilayani Mpanda
ambae jina lake nae limehifadhiwa alikutwa akimiliki bunduki
aina ya SMG yenye namba 1954 KO 3927 PNB na risasi 15
za bunduki aina ya SAR “alisisitiza
Alisema tukio jingine lilitokea hapo Novemba Mosi mwaka huu saa
12.30 osi jioni kijijini Kamsisi katika wilaya ya Mlele
mtu mmoja ambae hakufahamika alisalimisha bunduki aina ya
SMG yenye namba 1953MM 3468 kwa kuitupa nje ya mlango
wa nyumba ya Mwenyekiti wa kijiji hicho .
Siku hiyo hiyo huko katika Kijiji cha Utende Tarafa ya
Inyonga mtu asiye fahamika alisalimisha bunduki aina ya
SMG yenye namba 0957 ikiwa na magazine moja isiyokuwa na
risasi wala mtu huyo aliyesalimisha silaha hiyo hakuacha ujumbe
wowote wa maandishi “alisema .
Kamanda Nyanda alisema Novemba 02 katika kijiji cha Itenka,
Ofisa Mtendaji wa Kata ya Itenka wakati akiwa afisini kwake
alifika Mwenyekiti wa Kitongoji cha Kaderema akiwa na silaha
iliyotengenezwa kienyeji ‘gobori” ambayo ilisalimishwa na mkazi
wa kijiji hicho ambae alikuwa akisakwa na Polisi kwa kuhofia
kukamatwa na silaha hiyo alimpa mkewe ndio aikabidhi kwa
Mwenyekiti wa Kitongoji na yeye kutokomea kusiko julikana .
Kwa mujibu wa Nyanda katika kijiji cha Mtakuja Kata ya
Nsekwa mtu mmoja alisalimisha bunduki aina ya gobori kwa
Mwenyekiti wa kijiji hicho na kueleza nia yake ya kuachana na
kufanya ujangili huku akiwa ameambatanisha na risti
aliyolipia silaha hiyo ya mara ya mwisho yenye thamani ya Sh
3,000 - mwaka 2007 katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda .
Kamanda Nyanda aliomba jamii kuendelea kushirikiana na Jeshi
la Polisi katika kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu
kwani lengo kubwa ni kuona kwamba mkoa huo unakuwa salama
zaidi .
Katavi yetu Blog
JESHI la Polisi mkoani Katavi imekamata bunduki risasi ita zikiwemo
SMG nne na risasi 15 za SAR.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi Damas Nyanda alisema
silaha hizo zilikamatwa katika msako maalumu uliofanyika katika
wilaya za Mlele na Mpanda mkoani huo katika kipindi cha Septemba na
Oktoba
Alisema alisema Septemba 02, katika kijiji cha Kalovya , Tarafa
ya Inyonga katika wilaya ya Mlele watu wawili ambao majina yao
yamehifadhiwa walikamatwa wakiwa wanamiliki bunduki aina ya SMG
isiyokuwa na namba kinyume cha sheria .
“Isitoshe Septemba 28 , saa mbili usiku lilifanikiwa mtu
anayeishi katika makazi ya Wakimbi ya Katumba wilayani Mpanda
ambae jina lake nae limehifadhiwa alikutwa akimiliki bunduki
aina ya SMG yenye namba 1954 KO 3927 PNB na risasi 15
za bunduki aina ya SAR “alisisitiza
Alisema tukio jingine lilitokea hapo Novemba Mosi mwaka huu saa
12.30 osi jioni kijijini Kamsisi katika wilaya ya Mlele
mtu mmoja ambae hakufahamika alisalimisha bunduki aina ya
SMG yenye namba 1953MM 3468 kwa kuitupa nje ya mlango
wa nyumba ya Mwenyekiti wa kijiji hicho .
Siku hiyo hiyo huko katika Kijiji cha Utende Tarafa ya
Inyonga mtu asiye fahamika alisalimisha bunduki aina ya
SMG yenye namba 0957 ikiwa na magazine moja isiyokuwa na
risasi wala mtu huyo aliyesalimisha silaha hiyo hakuacha ujumbe
wowote wa maandishi “alisema .
Kamanda Nyanda alisema Novemba 02 katika kijiji cha Itenka,
Ofisa Mtendaji wa Kata ya Itenka wakati akiwa afisini kwake
alifika Mwenyekiti wa Kitongoji cha Kaderema akiwa na silaha
iliyotengenezwa kienyeji ‘gobori” ambayo ilisalimishwa na mkazi
wa kijiji hicho ambae alikuwa akisakwa na Polisi kwa kuhofia
kukamatwa na silaha hiyo alimpa mkewe ndio aikabidhi kwa
Mwenyekiti wa Kitongoji na yeye kutokomea kusiko julikana .
Kwa mujibu wa Nyanda katika kijiji cha Mtakuja Kata ya
Nsekwa mtu mmoja alisalimisha bunduki aina ya gobori kwa
Mwenyekiti wa kijiji hicho na kueleza nia yake ya kuachana na
kufanya ujangili huku akiwa ameambatanisha na risti
aliyolipia silaha hiyo ya mara ya mwisho yenye thamani ya Sh
3,000 - mwaka 2007 katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda .
Kamanda Nyanda aliomba jamii kuendelea kushirikiana na Jeshi
la Polisi katika kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu
kwani lengo kubwa ni kuona kwamba mkoa huo unakuwa salama
zaidi .
0 comments:
Post a Comment