Home » » POLISI KATAVI - OLE WAO WATAKAO ANDAMANA .

POLISI KATAVI - OLE WAO WATAKAO ANDAMANA .


   Na   Walter  Mguluchuma.
  Jeshi  la  Polisi  Mkoa wa  Katavi  limepiga  marufuku  kwa  vyama  vyote vya  siasa    vilivyopo  katika  Mkoa huu kutofanya  maandamano ,vikao  na  mikutano   mpaka hapo  yatakapoka  maelekezo   mengine kutoka   jeshi la  polisi  kutokana hali ya  usalama.
 Agizo  hilo  lilitolewa  hapo   jana  na   Kamanda wa  Jeshi  la   Polisi wa   Mkoa  wa      Katavi   Damas  Nyanda   mbele  ya   wandishi wa   Habari   ofisini   kwake  katika   Mtaa wa    Kasimba .
   Kwa  mijibu  wa  Kamanda   Damas  agizo  hilo    ni kutokana  na  maandamano  hayo  kuwa  na   viashiria   vya  uchochezi  kwa   wananchi   dhidi ya  Serikali  na  kunaweza  kutokea   usababishaji wa  uvunjifu wa   amani .
  Alisema   Jeshi  la  Polisi   Mkoa wa   Katavi  linatowa  onyo  kwa  mtu   au  kikundi  cha watu  kutojihusisha  kwa   namna  yoyote   ile  katika   kuratibu ,kuandaa  ama  kushiriki  katika  vikao ,mikutano  na  maandamano  ya  vyama   vya   siasa  na  vitendo  vyovyote   vile  vya  fujo ,ama  vitisho   vinavyoweza  kusababisha  uvunjifu wa  amani .
Kamanda   Damas   Nyanda    alieleza   Jeshi  la  Polisi   halitasita   kumchukulia   hatua   kali  za  kisheria   mtu  au  kikundi   chochote cha  watu  kitakacho   kaidi   igizo   hilo  lililotolewa  na   Jeshi  la  Polisi .
 Aliwataka  wananchi  kuendeleza   ushirikiano   mwema kwa  jeshi la  Polisi   katika  kutowa  taarifa  za  mtu  ama   vikundi  vya  aina  yoyote  vya   watu    vinavyojihusisha  kuratibu na  kupanga  kushiriki  katika  vikao    ,mikutano na   maandamano  ya  vyama vya  siasa  yenye  njama  za  kufanya   vitendo    vitakavyo   pelekea   uvunjifu wa   amani  wa  aina  yoyote  ili  hatua  kali zishukuliwe   dhidi   yao    mapema   iwezekanavyo .
 Aliwaomba  Raia  wema   wenye   mapenzi  mema   na   nchi ya   Tanzania  ambao  wanapenda   hali ya  ulinzi  na  usalama   kuendelea  kutamalaki  waendelee  kudumisha   mshikamano  wao kwa kutowa taarifa   kwenye  vyombo   vya  dola  zitakazoweza  kudhibiti   vitendo   vyote    vya   kihalifu   vitakavyopelekea  kuzorota  kwa  amani  na  usalama wa  Mkoa wa  Katavi .

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa