Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Na Walter Mguluchuma
Katavi yetu Blog
Mtu mmoja aliiyejulikana kwa jina la Gidison Visent 32 Mkazi wa Kijiji cha Katuma Tarafa ya Mwese Wilaya ya Mpanda ameuawa kwa kuchomwa na kisu kifuani na Mohamed Muna Mratibu wa Elimu wa Kata ya Katuma baada ya kumkuta akifanya mapenzi na mke wake ndani ya chumba chake cha kulala.
Kamanda wa Jeshi la polisi Mkoa wa Katavi Dhahiri Kidavashari aliwaambia waandishi wa Habari jana kuwa tukio hilo lilitokea hapo juzi mida ya saambili na nusu katika Kijiji hicho cha Katuma nyumbani kwa mtuhumiwa Muna.
Siku hiyo ya tukio mtuhumiwa alimkuta marehemu akiwa ndani ya nyumba yake chumbani huku akiwa anafanya mapenzi tendo la ndoa na mke wake anaitwa Ester Kasansa 36.
Alisema kitendo hicho cha kumfumania mkewe akiwa anafanya mapenzi na marehemu kilimkasirisha mtuhumiwa na ndipo alipoamua kumchoma kisu marehemu na kufariki Dunia hapo hapo na kasha alikimbia.
0 comments:
Post a Comment