Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Na Walter
Mguluchuma
Katavi yetu Blog
Waombolezaji
waliokuwa kwenye msiba wa marehemu aliyekuwa akijulikana kwa jina moja laDanie uliokuwa katika Mtaa wa Uwanja wa Ndege Mjini
Mpanda katika hari ambayo
hawakuitarajiwa walishikwa na mshituko
mkubwa baada ya muda wa kumwaga kabla ya mazishi baada ya
kufunuliwa sanduku lililokuwa
linatakiwa kuwemo mwili na kukutwa likiwa na sanduku tupu bila mwili wa marehemu .
Tukio hilo
la aina yake ambalo lilisimua watu wengi wa Manispaa ya
Mpanda lilitokea hivi karibuni katika mtaa wa Uwanja wa Ndege .
Siku hiyo ya
tukio waombolezaji hao walikuwa wako
msibani katika mtaa huwo wakiwa wanausubilia mwili wa marehemu Daniel uletwa hapo kwa ajiri ya mazishi ukiwa
unatokea chumba cha kuifadhi maiti
katika Hospitali ya Wilaya ya Mpanda
ulikokuwa umehifadhiwa kwa muda wa siku mbili .
Akielezea tukio
hilo mmoja wa wanafamili Azack Makanyaga
alisema kuwa yeye ndiye aliyepewa
jukumu na mama mkwe wa marehemu kushughulikia
taratibu za kuuchukua mwili wa marehemu
katika chumba cha kuifadhi maiti
cha Hospitali ya Wilaya ya Mpanda.
Alisema alifika kwenye chumba hicho cha
kuifadhia maiti huku akiwa na baadhi ya
waombolezaji na wakiwa wamebeba jeneza ambalo waliingia nalo ndani na kisha walimuacha yeye ndani ya
chumba hicho kwa ajiri ya kuocha mwili huo wa marehemu .
Makanyaga
alieleza wakati alipokuwa akiwa anajiandaa kuosha mwili wa marehemu alitoka
nje ya chumba hicho cha kuhifadhi maiti na kwenda kwenye geti la walinzi
na kuwaonyesha kibali cha kuutolea mwili wa marehemu kwenye chumba cha kuifadhi
maiti.
Kitendo hicho cha
Makanyaga kwenda kwenye geti la
walinzi kilichochukua muda mrefu kiliwafanya wale waombolezaji waliokuwa nje
ya chumba cha kuifadhi maiti waamue kuingia ndani na kuchukua jeneza
wakijua kuwa mwili wa marehemu umo ndani ya jeneza na kisha walilipatia jeneza na kuelekea msibani katika mtaa wa uwanja wa Ndege kwa ajiri ya mazishi.
Baada ya kufika
msibani hapo taratibu za mazishi zilanza
ambapo waombolezaji walitangaziwa kuwa
kabla ya mwili wa maremu hauja pelekwa
makaburini waombolezaji watauaga mwili wa Marehemu na wataanza kuaga wanaume
kisha wanawake .
Jeneza hilo
lilifunguliwa kwa ajiri ya kuaga mwili wa marehemu ndipo waombolezaji
walikuwepo msibani hapo waliposhikwa na mchangao kuona jeneza likiwa tupu bila kuwemo ndani ya
marehemu ndani ya jeneza hilo .
Hari hiyo
iliwafanya ndugu wa marehemu waanze
kuwahoji watu waliokuwa wamewagiza waufatie mwili wa marehemu kwenye chumba cha
kuifadhi maiti kuwa mwili wa marehemu wameupeleka wapi.
Kufatia
majadiliano ya muda mrefu walifikia uamuzi wa kurudi kwenye chumba cha kuifadhi
maiti katika hospitali ya Wilaya ya Mpanda na
waliweza kuukuta mwili huo ukiwa ndani ya chumba hicho na ndipo
walipoupakia kwenye gari na walipofika
kwenye geti la walinzi walizuiwa na
walinzi kuutowa mwili huo kwa kile walinzi walichodai kuwa mwili wa marehemu
walichauchukua na huo sio mwili wa ndugu yao.
Uongozi wa
Hospitali uliingilia kati kutatua tatizo hilo la ndugu wa marehemu na walinzi
kwa kuwaruhusu ndugu wa marehemu kuuchukuwa mwili wa marehemu na mazishi yake yliweza kufanyika siku hiyo
hiyo majira ya saa moja jioni
0 comments:
Post a Comment