Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi, Dhahiri Kidavashari.
Askari polisi Konstebo Norbert Chacha (25) ameuwawa kwa kupigwa risasi kifuani na mgongoni wakati akifanya ujambazi.
Mauaji ya askari huyo yalitokea usiku wa kuamkia juzi usiku wa
manane katika kijiji cha Ibindi, wilayani Mlele, akiwa na watu wengine
ambao walikuwa wamekwenda kufanya ujambazi kwenye nyumba ya
mfanyabiashara wa madini ya dhahabu kijijini hapo.
Diwani wa Kata ya Machimboni, Raphael Kalinga, aliwaambia waandishi
wa habari kuwa askari huyo akiwa na kundi la majambazi wenzake, ambao
idadi yao haikufahamika, walifika kijijini hapo kwa lengo la kumvumia na
kumpora mfanyabiashara huyo, Daniel John.
Alisema baada ya kufika nyumbani kwa mfanyabiashara huyo, walivunja mlango wa mbele, wakati mfanyabiashara huyo akiwa amelala.
Majambazi hayo, alisema baada ya kuvunja mlango, waliingia ndani
na mfanyabiashara aliwauliza ni kinanani na ndipo walipomwamuru
asipige kelele vinginevyo watamuua.
Kalinga ambaye ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo,
alisema kutokana na amri hiyo, John alichukua bunduki yake ya shotgun
na kufyatua risasi ambayo ilimpiga askari huyo kifuani na mgongoni na
kufa hapo hapo.
Alisema majambazi wenzake ambao walikuwa na mapanga na shoka
baada ya kuona mwenzao kapigwa risasi na kufa waliamua kumbeba marehemu
na kwenda kumtupa kichani umbali wa mita 200 kutoka kwenye eneo la tukio
na kisha walitokomea kusiko julikana.
Wakazi wa Kijiji hicho walifika nyumbani kwa mfanyabiashara huyo
na kukuta michirizi ya damu na ndipo walipoamua kuifuata ilikokuwa
inaelekea.
Alisema wanakijiji waliendelea kuifuata michirizi hiyo na
walipofika umbali wa mita 200 kutoka nyumbani kwa John, waliuona
mwili wa askari polisi huyo ambaye alikuwa amefariki dunia kutoa
taarifa polisi wilaya ya Mpanda.
Polisi walifika kwenye eneo hilo baada ya muda mfupi na ndipo
walipomtambua marehemu kuwa ni askari polisi wa kituo cha cha wilaya
ya Mpanda .
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi, Dhahiri Kidavashari,
amethibitisha kuuwawa kwa askari huyo kuwa alipigwa risasi akiwa katika
harakati za kufanya ujambazi na kupora .
Alisema mwili wa marehemu bado umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika Hospitali ya Wilaya ya Mpanda .
Kabla ya tukio hilo, kulikuwa na malalamiko kutoka kwa wananchi wa
mkoa wa Katavi waliokuwa wakiwatuhumu baadhi ya askari polisi kuhusika
katika matukio ya ujambazi na uporaji mkoani hapa.
CHANZO:
NIPASHE
0 comments:
Post a Comment