Na Walter
Mguluchuma
Katavi
Mwanafunzi
wa Darasa la nne
wa Shule ya Msingi Mwamkulu Manispaa ya Mpanda
Mkoa wa Katavi Manisiter
Joe (14) ambae wazazi wake
walitaka kumwozesha kwa nguvu na ndoa yake kuvunjika kabla haija fungwa
amefanya mtihani wa Taifa wa Darasa
la nne chini ya usimamizi wa ofisi
ya maendeleo na ustawi wa Jamii ya
Manispaa ya Mpanda
Mwanafunzi
huyo alikuwa ameachishwa na masomo
na wazazi wake na kuamua
kumwozesha kwa aliyewahi kuwa
mwanafunzi mwenzake wa shule hiyo baada ya wazazi wake kuwa wamepokea
mahari ya Ng’ombe 15
Hivi
karibuni ofisi ya Elimu
ya Manispaa ya Mpanda
kwa kushilikiana na jeshi
la Polisi Mkoa wa
Katavi walifanikiwa kusitisha ndoa ya
mwanafunzi huyo aliyetaka
kuozeshwa kwa nguvu ya
wazazi pasipo kuwa na ridhaa yake
mwenyewe muda mfupi kabla ya ndoa yake
kimila kufungwa katika Kijiji
cha Mwamkulu Wilayani
hapa na kijana huyo huku akiwa
amevarishwa shela tayari tayari kwa ndoa kufungwa kwa ndoa hiyo ilivutia hisia za watu wengi wa Mkoa wa Katavi na nje ya
Mkoa
Akizungumza na Waandishi wa Habari hapo
jana Ofisini kwake
Afisa Elimu wa Manispaa ya Mpanda
Vicent Kayombo alisema kuwa Mwanafunzi
huyo baada ya kuwa ametendewa hivyo na baba yake
mzazi Manispaa ya Mpanda iliamua kuchukua jukumu la
kumuumishia yule ya Msingi Azimio ambayo
ipo katikati ya Manispaa ya Mpanda huku
akiwa chini ya uangalizi wa idara ya
maendeleo na ustawi wa jamii
Kayombo alifafanua kuwa pamoja na kuwamwamishia kwenye
shule hiyo amelazimika
kwenda kufanya mtihani wa Taifa wa Darasa
na nne kwenye shule yake ya zamani ya Mwamkulu kwa kuwa alikuwa
amesajiriwa kufanyia mtihani kwenye
shule hiyo
Alisema
ameondoka leo yaani
jana kwenda kufanya mtihani huo
huku akiwa amesindikizwa na Afisa
Maendeleo wa Ustawi wa Jamii wa Manispaa ya Mpanda
ambae akuwa nae huko hadi atakapo kuwa amemaliza
mitihani yake na kisha
atarudi nae mjini
Mpanda
Alieleza
baada ya kumaliza mitihani
hiyo ataendelea na
masomo kwenye shule ya Msingi Azimio
na sio Mwamkulu tena
kwani Manispaa ya Mpanda imeisha
chukua jukumu la kumuhamisha
kwenye shule yake za zamani
Alisema
pamoja na baba
mzazi wa mtoto huyo ambae alitoroka
baada ya jaribio lake
la kutaka kumwozesha
kushindikana mwanafunzi huyo
ameonyesha nia ya
kuendelea na masomo
na amemwakikishia Afisa
Elimu wa Manispaa kuwa
lazima atafaulu mtihani wa Taifa wa Darasa la
nne na ule wa kumaliza darasa
la saba
Pamoja na juhudi
hizo za kumnusuru mwanafunzi
huyo baba mkubwa wa
mtoto huyo nae pia
ameonyesha nia za kutaka
kumchukua mtoto huyo ili
aweze kuendelea na
masomo katika shule
hiyo ya Azimio na amepinga
vikali kitendo hicho cha mdogo wake alisema
Kayombo
Alisema
wanaangalia namna ya kuweka
utaratibu wa kumkabidhi
baba yake mkubwa na mtoto huyo ila kwa masharti ya kuhakikisha mwanafunzi huyo anaendelea na masomo yake kama
kawaida
Manispaa ya
Mpanda kwa kipindi cha miaka miwili mfululizo sasa ndio inayoongoza kwa matokeo ya ufaulu wa wanafunzi wa Darasa
la saba Kitaifa
0 comments:
Post a Comment