Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Na Walter
Mguluchuma
Katavi
Mgombea Ubunge
wa Jimbo la Nsimbo Wilayani Mlele
Mkoa wa Katavi Elias Kifunda (ACT WAZALENDO TANZANIA) amewataka viongozi
wa Serikali wadini na wavyama vya siasa
kuwaelimisha watu umuhimu wa uzazi wa mpango
Kifunda ambae ni Wakili wa kujitegemea aliyasema hayo hapo
jana ofisini kwake katika eneo la madukani mjini
Mpanda wakati akizungumza na mwandishi wa gazeti hili
Alisema kumekuwepo na ongezeko kubwa la watu hapa
Nchini za zaidi ya nusu ya watu hao ni wale ambao
wanaumri mdogo na
matokeo yake Serikali imekuwa
ikibeba mzigo mkubwa wa kuwaudumia watu
kwa kuwa ni jukumu la Serikali kuhudumia watu
Alifafanua kuwa idadi ya watu
ni lazima ilingane na uwezo
wa Serikali wa kuwahudumia
watu wake katika maswala mbalimbali
kama vile Elimu Afya Maji na huduma nyinginezo
Alisema uzazi wa mpango ni swala muhimu sana ingawa
swala hilo lilikuwa
halijawekwa mkazo kitachotakiwa sasa hivi
ni watu kupewa elimu ya madhara ya kuzaa bila
mpangilio na itolewe mashuleni kwenye vyuo na
katika vituo vya afya na zahanati
Hivyo
viongozi wote wa Serikali Dini na
vyama vya siasa wanalo jukumu
la kuelimisha watu umuhimu wa
uzazi wa mpango na ndio maana zipo baadhi ya nchi zimetunga sheria
za idadi ya watu ambao mtu anatakiwa kuzaa
Alisema
uzazi wa mpango unasaidia
mtu kuzaa watoto ambao
anakuwa na uwezo nao wa
kuwahudumia mahitaji ya lazima ya binadamu
Kifunda
alisema watoto wachanga ni kundi
ambalo wanaathilika zaidi na
maradhi kwani watoto
wachanga hawezi kujihimili
wenyewe hivyo endapo atachaguliwa
kuwa
Mbunge ataakikisha huduma za
mama na watoto
wachanga zinaimarika katika jimbo lake na Taifa kwa ujumla
0 comments:
Post a Comment