Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Vurugu hiyo ilisababishwa na wafuasi hao wa Chadema na CCM kugombania “kijiwe” kimoja kilichopo eneo la Soko Kuu mjini hapa kutundika bendera za vyama vyao vya saisa na mabango ya wagombea wao .
Mkasa huo
ulitokea saa moja na nusu usiku
katika eneo la Soko Kuu mjini
Mpanda katika Mtaa wa Kashaulili baada
ya wafuasi wa CCM wakiongozana na Mwenyekiti wa Mtaa wa Kashaulili , Mage
Kitunguru ( “Mhaya” ) kufika kwenye kijiwe hicho
wakiwa na bendera za CCM na mabango
ya wagombea wao wakitaka kutundika .
Kwa mujibu wa
mashuhuda walikuwa katika eneo hilo
wanaeleza kuwa kitendo hicho cha wafuasi
hao wa CCM na mwenyekiti wao wa Mtaa kutaka
kutundika bendera za CCM katika kijiwe cha kiliwasirisha
sana wakiwadai kuwa kijiwe hicho
ni mali ya Ukawa hivyo CCM
hawastahili kutundika bendera zao
wala kupandika mabango ya wagombea wao .
“ Wafiasi wa vyama hivyo viwili vya siasa walianza kurushiana maneno makali wakitishiana maisha huku wakizomeana .... hali iliyosababisha umati wa watu kukusanyika katika eneo hilo na kuhatarisha uvunjifu wa amani na utulivu wa eneo hilo “ alisema mtoa taarifa kwa masharti ya kutoandikwa jina lake .
Askari polisi wakiwa na silaha walifika katika eneo hilo la tukio lakini walipojaribu kuwatuliza wafuasi wenye hasira wa CCM na Chadema kwa amani waliendelea kulumbana na kutishiana maisha .
Inadaiwa kuwa ndipo askari polisi hao walipolazimika kufyatua risasi hewani ili kuwatawanya wafuasi hao ambao walitimua mbio wakitoka eneo hilo la tukio .
“ Wafiasi wa vyama hivyo viwili vya siasa walianza kurushiana maneno makali wakitishiana maisha huku wakizomeana .... hali iliyosababisha umati wa watu kukusanyika katika eneo hilo na kuhatarisha uvunjifu wa amani na utulivu wa eneo hilo “ alisema mtoa taarifa kwa masharti ya kutoandikwa jina lake .
Askari polisi wakiwa na silaha walifika katika eneo hilo la tukio lakini walipojaribu kuwatuliza wafuasi wenye hasira wa CCM na Chadema kwa amani waliendelea kulumbana na kutishiana maisha .
Inadaiwa kuwa ndipo askari polisi hao walipolazimika kufyatua risasi hewani ili kuwatawanya wafuasi hao ambao walitimua mbio wakitoka eneo hilo la tukio .
“Polisi
walipoaanza kufyatua risasi hewani wafanyabiashara walifunga maduka yao
pia wauza matunda na mboga mboga
waliokuwa wakifanya biashara zao jirani
na eneo hilo la tukio
walilazimika kutimua mbio wakihofia usalama wa maisha yao “ alisema mkazi wa Mtaa wa kashaulili aliyejitambulisha
kwa jina la Adam Michael
Ofisa wa Jeshi
la Polisi kwa masharti ya kutoandikwa gazeti kwa kuwa si msemaji amekiri
kutokea kwa tukio hilo akisisitiza kuwa hakuna
maafa yeyote yaliyotokea kwamba jeshi hilo lilifanikiwa
kumkatamata mtu moja aliyejulikana kwa jina moja la Elick Mkazi wa
Mtaa w Majengo Mjini hapa
Katibu
wa CHADEMA wa Mkoa wa Katavi Almasi Ntije alisema kuwa Chama chake
kimesikitishwa na kitendo kilichofanywa na wafuasi wa CCM cha kutaka
kuweka bendera na mabango ya wagombea wao kwenye jiwe cha wafuasi wa
CHADEMA(UKAWA)
Alisema
tume ya uchaguzi imeisha towa maelekezo kwa vyama vyote kufanya
shughuli zao mwisho ni saa kumi na mbili jioni hivyo ameshangazwa na
kitendo hicho kufanywa na wafuasi wa CCM majira ya saa moja na nusu
huku wakijua ni kinyume cha kanuni za tume ya uchaguzi
Nae Mwenyekiti wa CCM wa Wilaya ya Mpanda Beda Katani alikili kuwepo kwa vulugu hizo za wafuasi wa vyama hivyo
Alisema
anasubiri apewa taarifa nzima ju ya tukio hilo ndipo atakapokuwa
tayari kuzungumzia tukio hilo kama Mwenyekiti wa Chama
0 comments:
Post a Comment