N a Walter
Mguluchuma
Katavi
Jumla ya
Wanawake 255 wamefariki Dunia Mkoani Katavi katika kipindi cha mwaka
2014 kutokana na matatizo ya uzazi kwa kila
vizazi hai laki moja
Hayo yalielezwa hapo jana na Mkuu wa Mkoa
wa Katavi Dr Ibrahimu
Msengi kwenye hotuba yake ya
uzinduzi wa huduma za
uzazi wa mpango iliyosomwa kwaniaba yake na Kaimu Mkuu wa Mkoa
wa Katavi Paza Mwamlima ambae ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda kwenye sherehe ya uzinduzi huo iliofanyika
katika uwanja wa shule ya Msingi Kashaulili mjini Mpanda na huhudhuriwa na
maefu ya wakazi wa Mkoa wa Katavi
Alisema Katika Mkoa wa Katavi kiwango
cha vifo vya wanawake
vinavyotokana na matatizo ya uzazi kwa kipindi cha mwaka jana wa
2014 ilikuwa ni 255 kwa kila vizazi hai
laki moja
Idadi
hii ni kwa wale wanawake waliotolewa
taarifa katika vituo vya kutolea
huduma na kutoka katika
ngazi ya jamii hivyo idadi hiyo
inaweza ikawa ni kubwa zaidi kwani ziko
taarifa nyingine za vifo vya wanawake taarifa zake hazitolewi kwenye ngazi husika hasa kwenye maeneo ya
vijijini ambako kunafikika kwa shida
Dr Msengi alieleza kiwango
cha Kitaifa cha vifo
vya wanawake vinavyotokana na matatizo
ya uzazi ni 454 kwa
kila vizazi hai laki moja
Utafiti kuhusu
afya ya uzazi wa mwaka 2010 (Tanzania
Demographic Survery) inakadiliwa
kuwa asilimia 23 ya wanawake wenye umri
wa miaka 15 mpaka 19 na
asilimia 54 ya wenye umri
wa miaka 19 mpaka 24 tayari wana watoto na mimba
katika umri mdogo huchangia vifo
mara mbili hadi tano
ya vifo vitokanavyo na uzazi
Alisema
kiwango cha utumiaji wa njia
za uzazi wa mpango katika
Mkoa wa Katavi kwa mwaka 2014 ilikuwa ni asilimia 38.4
tu kiwango hicho
kiko chini sana ukilinnganisha na kiwango cha Kitaifa
kwani kiwango cha Taifa ni
asilimia sitini
Dr Msengi
alieleza wapo watu wanaamini kuwa kuzaa watoto wengi ni utajiri
na wengine wanaamini
mwanamke ni chombo cha kuzaa watoto tuu hivyo ni vizuri watu wakaepukana na mila hizo
potofu
Kwa upande
wake Mkurugenzi Mkuu wa Rasilamali watu wa Marie
Stopes Tanzania (MST) Eliy Reweta
ambae alimwakilisha Mkurugenzi Mkuu alieleza kuwa Marie Stopes
inatowa huduma hiyo ya uzazi wa mpango
wa bure
lengo ni kumwezesha kila mmoja
kuchagua njia ya uzazi
ya mpango anayohitaji hasa miongoni
mwa vijana
Alifafanua kuwa
vijana wanaweza kudhani
kuwa huduma za uzazi wa mpango
ni kwa ajiri ya watu wanaoishi
katika ndoa wakati ni muhimu wao kuepuka
mimba zisizotakiwa hata kabla ya ndoa
Mwenyekiti wa
Halmashauri ya Mji wa Mpanda Enock
alisema kuwa uzazi wa mpango ni jambo la muhimu sana kwenye maisha ya
Binadamu kwani husaidia kupunguza vifo
vya watoto wachanga ambao mama zao
hupata ujauzito wakati wakiwa bado wadogo
Alisema pia uzazi wa mpango husaidia watoto
kuzaliwa kwa kuachiana nafasi na
kunyonyeshwa kwa muda wa miezi
inayotakiwa na mama zao
Nae mshindi wa
taji la Miss Marie Stopes katika
mashindano ya Miss Tanzania
yaliofanyika mwezi Septemba mwaka jana
Doreen Benne alieleza kuwa
uzazi wa mpango unamkinga
mwanamke asipate mimba zisizotarajiwa na
kumwepusha na kuingia kwenye
mtego wa kutowa mimba kusiko salama
Napia uzazi wa mpango unamsaidia mwanamke kuishi maisha
mazuri yale ambayo anayoyataka mwenyewe kadri atakavyo kuwa amejipangia mwenyewe alisema Doreen
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
0 comments:
Post a Comment