Home » » MAJAMBAZI YA PORA KWA KUTUMIA SILAHA YA KIVITA

MAJAMBAZI YA PORA KWA KUTUMIA SILAHA YA KIVITA


Na  Walter  Mguluchuma
Katavi
 Watu watatu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi wakiwa na silaha ya Kivita aina ya SAR  wamevamia Kitongoji cha  Ruhafe  Kijiji cha Vikonge  Wilaya ya Mpanda Mkoa hapa  na kuwapora wafanya biashara wa maduka kumi na mbili  vitu mbalimbali  baada ya kufyatua  risasi hewani  ya kuwatishia
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi Dhahiri Kidavashari aliwaambia waandishi wa Habari   kuwa tukio hilo la  unyang’annnnnyi wa kutumia silaha lilitokea hapo jana majira ya saa mbili na robo usiku katika Kitongoji hicho cha Ruhafe
 Katika tukio hilo majambazi hao walivamia maduka 12 ya wafanyabiashara    baada ya kuwatisha kwa kufyatua Risasi hewani kwa kutumia bunduki ya kivita aina ya SAR
Majambazi hao waliweza  kupora vitu mbalimbali  vikimemo  simu , Soral  panal ,lap top , bidhaa za  dukani  na kisha baada ya kupola  waliendelea kuwafyatua Risasi zisizo na idadi  hewani  za kuwatisha wananchi wa eneo hilo na kisha walitokomea kusiko julikana
Kidavashari  aliwaambia waandishi wa Habari  kuwa  thamani ya  vitu hivyo  vyote vilivyopolwa  bado  haijajulikana  mpaka sasa 
 Alisema jeshi la Polisi kwa  kwa kushirikiana na Wananchi  na uongozi wa Kitongoji hicho  walifanikiwa   kumkamata  mtuhumiwa mmoja  kuhusika na tukio hilo  ambae alijulikana kwa jina la  Yusuph  Malaki (35) Mkazi wa Makazi ya Wakimbizi ya Katumba Wilaya ya Mlele
Mtuhumiwa  alikamatwa  akiwa na pikipiki  moja  aina ya  Sanlg   yenye namba za usajiri  T.209 CEB Ambayo ilikuwa ikitumiwa na majambazi hayo kwenye tukio hilo
 Kamanda Kidavashari alisema    juhudi  za kuwasaka   watuhumiwa  wengine waliohusika na tukio  hilo bado zinaendelea kwa polisi  kwa kushirikiana na Wananchi
 Mtuhumiwa  Yusuph  Malaki  bado anaendelea kushikiliwa na Polisi na atafikishwa Mahakamani  mara baada ya uchunguzi wa tukio hili utakapo kuwa umekamilika
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa