Na Walter
Mguluchuma
Katavi yetu blog
Mtu
mmoja aliyefahamika kwa jina la
Shija Ngasa (35) Mkazi wa Kijiji
cha Katuma Wilaya ya Mpanda Mkoa wa
Katavi ameuwawa kikatili kuchinjwa
shingo hadi kufa na watu wasio julikana wakati akiwa na familia yake nyumbani kwake
wakisubilia kula chakula cha jioni
Mauwaji hayo ya
kutisha na yakikatili yalitokea hapo
juzi majira ya saa mbili usiku nyumbani
kwa marehemu Shija Ngasa katika Kijiji cha Katuma ambapo
marehemu alikuwa akiishi na familia yake
Kamanda wa Polisi
wa Mkoa wa Katavi Kamishina msaidizi mwandamizi aliwaambia jana waandishi wa Habari kuwa
marehemu huyo aliuwawa wakati akiwa nyumbani kwake yeye na familia
yake wakati wakiwa wanasublia kula chakula
cha usiku kilichokuwa
kinaandaliwa jikoni na mke wake
Alisema wakati
wakiwa wanasubilia chakula hicho ghafla
walitokea watu wawili wasio fahamika
huku wakiwa wamefunika uso
wao na mmoja wa watu hao alikuwa
ameshika shoka mkononi
Aliwaeleza
waandishi wa Habari kisha watu hao walimvamia marehemu
na kuanza kumchinja kwa shoka huku watoto wake wawili wakiwa wanashuhudia kitendo hicho cha mauwaji ya kikatili
Kidavashari alisema
watoto hao wa marehemu
waliendelea kupiga mayowe ya kuomba msaada kwa majirani na
ambao walifika kwenye eneo hilo
na kukuta watu hao wameisha tokomea
kusiko fahamika huku mwili wa marehemu ukiwa unagalagala chini
Alisema majirani walikwenda kutoa taarifa
za mauwaji hayo kwa viongozi wao wa
Kijiji ambao nao walitoa taarifa kwa jeshi la Polisi Wilaya ya Mpanda
Chanzo cha
mauwaji hayo ya kikatili bado hakija julikana na mpaka sasa
hakuna mtu wala watu waliokamatwa kuhusiana na
mauwaji hayo
Aidha jeshi la
Polisi kwa kushirikiana na uongozi wa Kijiji hicho cha Katuma wanaendelea
na jitihada za kuwasaka na
kuwabaini na kuwakamata wale
wote waliohusika katika mauwaji
hayo
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
0 comments:
Post a Comment