Home » » HOT NUUZ: MISA YA PASAKA YASIMAMA KWA MASAA MANNE NI BAADA YA KWAYA MBILI KUGOMBANIA KUIMBA.

HOT NUUZ: MISA YA PASAKA YASIMAMA KWA MASAA MANNE NI BAADA YA KWAYA MBILI KUGOMBANIA KUIMBA.


Na   Walter  Mguluchuma 
Katavi
Waumini wa Kanisa Katoliki   Kigango cha Utende Porokia ya Inyonga Jimbo Katoliki la Mpanda  wamelazimika   kushindwa kusali ibada ya  misa ya sikukuu ya Pasaka kwa muda masaa manne  baada ya kutokea vulugu za kwaya mbili za Kigango hicho kugombania kuimba   kwenye Ibada ya misa ya Pasaka  na kumtishia  kupiga kwa mawe Katekisita wa Kigango  hicho
 Tukio hilo  llitokea hapo juzi majira ya saa nne asubuhi  ndani ya Kanisa la Kigango cha utende muda mfupi baada ya kuanza kwa ibada ya misa ya sikukuu ya Pasaka iliyokuwa ikiongozwa na Katekisita wa Kigango hicho Credo  Mwakipanda
Kwa mujibu wa makamu  mwenyekiti wa Kigango hicho Abel Kalifumu alisema vurugu  hizo zilizihusisha  kwaya mbili za Mtakatifi Sesilia na Mtakatifu  Agusino
Alisema  uongozi wa Kigango hicho huwa wamaisha zipangia utaratibu  kwaya hizo wakati wa sikukuu kuimba  kwa  zamu   kwenye misa  moja
 Alifafanua siku hiyo ya Pasaka wanakwaya wa kwaya ya Mtakatifu Seselia walikataa wenzao wa kwaya ya Mtakatifu Agustino wasiimbe kwenye ibada hiyo kwa kile walichodai kuwa siku hiyo ilikuwa ni zamu yao kuimba peke yao
Alisema baada ya mabishano ya muda mrefu wa kwaya hizo muda wa kuanza ibada ulifika na Katekisita alipiga kengele kwa ajiri ya waumini ili waingie kanisani kwa kuanza ibada ya misaa ya Pasaka
 Wakati   Katekisita akiwa kwenye aktale kwa ajiri  kuendesha ibada  ghafla  kwaya hizo mbili kila mmoja  alianza kiimba  wimbo wake  kwa wakati mmoja hari ambayo ilipelekea kutokea hari ya kelele  kubwa ndani ya  kanisa hilo
Katikisa Credo alizisihi kwaya hizo  ziache vurugu iliibada iendelee kama  kawaida  lakini wanakwaya wa Mtakatifu Sesilia walimtishia Katekista kuwa endapo ataendelea na ibada watampiga kwa mawe
Kalifumu alieleza baada ya katekista kuona hari ya vurugu imekuwa kubwa alilazimika kusitisha ibada na kutoka nje  ambapo  alikuta hari ya vurugu ikiwa inaendelea na ndipo alipovua kanzu yake na kuwakabidhi  viongozi wa kigango ambao walimsihi  arudi kanisani  akaendelee na ibada hata hivyo wanakwaya wa Mtakatifu Sesilia waliendelea kumtishia kuwa akirudi kusalisha wanampiga mawe hari iliyomlazimu  amue kweda kwake
 Alisema  baada ya  katekista kuwa amekwenda nyumbani kwake viongozi wa kigango walimfuata  nyumbani kwake na kumsihi arudi lakini alikataa kata kata
Waumini wa Kanisa hilo baada ya kuambiwa kuwa  kateksta amekataa kurudi  waliteuwa wazee maarufu wa kijiji hicho ambao  waliongozana na viongozi wa kigango hicho na kumsihi kateksta arudi kanisani na kuendesha ibada  ombi ambalo katiksta Credo alikubali na kurudi kanisani majira ya saa saba na nusu mchana
Alisema baada ya kateksta kufika kanisani hapo aligonga kengele kwa ajili ya kuanza ibada ambapo waumini wakanisa hilo waliziamuru kwaya hizo zisiimbe kwenye ibada hiyo na  misa hiyo ilifanyika  bila kwaya yoyote ile kuimba waumini waliimba nyimbo za zamani


    

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa