Na Walter
Mguluchuma
Katavi
Jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi linamshikilia
mtu mmoja Mganga maarufu wa jadi kwa tuhuma za kumkamata akiwa na fuvu
la kichwa cha Binadamu akiwa ameligifadhi ndani ya choo
anachokitumia
Kamanda wa Polisi
wa Mkoa wa Katavi Dhahiri Kidavashari
aliwaambia waandishi wa habari
jana ofisini kwake kuwa mtuhumiwa Kabichi
Mhulu (39) Mkazi wa Kijiji cha Kakese Wilaya ya Mpanda Mkoa wa
Katavi alikamatwa hapo jana majira ya saa kumi na mbili jioni nyumbani
kwake katika Kijiji cha Kakese
Kwa mujibu wa
Kamanda Kidavashari mtuhumiwa huyo
alikamatwa na fuvu hilo la kichwa cha binadamu akiwa ame amelihifadhi ndani ya choo alichokuwa akikitumia
Kukamatwa kwa
mtuhumiwa huyo ambae ni mganga maarufu wa kienyeji kulitokana na taarifa
za raia wema ambao waliokuwa wametowa
taarifa kwa jeshi la polisi kuwa mganga huyo amehifadhi fuvu la kichwa ndani ya
choo chake
Alisema baada ya taarifa hizo kulifikia jeshi
la polisi lilifika katika Kijiji hicho cha Kakese na kisha walikwenda nyumbani
kwa mtuhumiwa kwa ajiri ya kumfanyia
upekuzi
Kidavashari
alieleza Polisi walifanya upekuzi kwenye
nyumba ya mtuhumiwa Kabichi Mhulu na waliweza kufanikiwa kumkamata
akiwa na fuvu la kichwa cha
binadamu akiwa amekihifadhi ndani ya choo
alichokuwa akikitumia
Alisema fuvu hilo alilokamatwa nalo alikuwa
akilitumia kwa ajiri ya wateja wake
waliokuwa wakifika hapo kwa ajiri
ya matibabu ambapo walikuwa wakilikalia fuvu hilo wakati
walipokuwa wakipatiwa matibabu yao
Mtuhumiwa
anaendelea kushikiliwa na polisi kwa
mahojiano zaidi na anatarajiwa
kufikishwa mahakamani mara baada ya upelelezi kukamilika ili
kujibu tuhuma inayomkabili
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
0 comments:
Post a Comment