Na Walter
Mguluchuma
Katavi
Mwanamke
mmoja Mkazi wa Kijiji cha Ugala Tarafa ya Ndurumo Wilaya ya Mlele Mkoaa wa Katavi amekamatwa
kwa tuhuma za kukamatwa akiwa na sare ya
Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na
sare ya askari za wanyama pori wa TANAPA
Mtuhumiwa huyo
mwanamke aliyekamatwa alijulikana kwa jina la Ester John(21) Mkazi
wa Kijiji hicho cha Ugala Wilaya ya Mlele
Kamanda wa Polisi
wa Mkoa wa Katavi Dhahiri Kidavashari aliwaambia waandishi wa habari hapo jana
kuwa mtuhumiwa Ester alikamatwa jana majira ya
saa kumi jioni wakati akiwa nyumbani kwake
Kidavashari
alisema muhumiwa huyo alikamatwa kufuatia taarifa za kutoka kwa raia wema ambao
walitowa taarifa kwa jeshi la Polisi kuwa mtuhumiwa huyo amekuwa akihifadhi
nguo hizo sare za jeshi na zimekuwa zikitumiwa na watu kwa ajiri ya kufanya
uharifu
Alisema baada ya taarifa hizo Polisi kwa
kushirikiana na Askari wa TANAPA walikwenda Kwenye Kijiji hicho cha Ugala kwa lengo la
kufutilia taarifa hizo
Kidavashari
alieleza baada ya kufika kijijini hapo
Askari hao walikwenda nyumbani kwa Mtuhumiwa Ester kwa lengo la kumpekua nyumba yake hiyo
Alisema
katika upekuzi walioufanya kwenye nyumba ya Mtuhumiwa Ester waliweza kumkamata akiwa na saruali
moja na shati moja la jeshi la wananchi wa
Tanzania(JWTZ) pamoja sare pea moja
za askari wa wanyama pori TANAPA
na vyuma viwili vya
kutengenezea risasi
Mtuhumiwa bado
anaendelea kushikiliwa na Polisi na atafikishwa mahakamani mara baada ya
uchunguzi wa tukio hilo utakapo kuwa umekamilika
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
0 comments:
Post a Comment