Home » » WAALIMU WALALAMIKIA KUWAFUNDISHA WANAONYONYESHA

WAALIMU WALALAMIKIA KUWAFUNDISHA WANAONYONYESHA


Na  Walter  Mguluchuma
Katavi yetu Blog
Baadhi ya  Walimu  wa shule za Sekondari  zilizopo  katika Halmashauri ya Mji wa Mpanda wanalazimika  kuruhusu wanafunzi   wanaonyonyesha  kuacha masomo  na kuruhusu kurudi nyumbani kwao kwenda kunyonyesha  watoto
 Mamalamiko hayo ya baadhi ya waalimu yalitolewa hapo jana na waalimu hao kwenye mkutano wao na Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dr Ibrahimu Msengi  uliofanyika  kwenye ukumbi wa shule ya Sekondari ya Mtakatifu Maria mjini hapa
Waalimu hao walisema  wamekuwa wakilazika kuwaruhusu wanafunzi wanaowafundisha  kuacha vipindi vya masomo darasani na kuwaruhusu warudi nyumbani kuwanyonyesha  watoto wao nyumbani   pindi wanapokuwa wameomba ruhusa hiyo
Mmoja wa waalimu wa shele ya Sekondari  Nsemlwa mwalimu  Zakaria  Leonald  alisema yeye  huwa analazimika kumpatia  ruhusa mwanafunzi mmoja ambae  huwa anakuja shuleni huku  akiwa amemuacha mtoto anae nyonya nyumbani
Alisema  mwanafunzi huyo  huwa anakuwa analalamika darasani wakati  vipindi vinapokuwa vinaendelea   kuwa maziwa yake  yanamuuma  kwa kuwa yanakuwa yamejaa kutokana na kuto na kuwa yamejaa kutokana na kutomnyonyesha mtoto wake kwa muda mrefu
 Alisema  hali hiyo ya kuwachannnnnnnnganya wanafunzi ambao waliozaa na ambao hawaja zaa imekuwa ikiwaathili baadhi ya wanafunzi wa wasichana
 Alifafanua  kuwa serikali iangalie utaratibu wa  kuwa na shule maalumu kwa ajiri ya  wanafunzi  wale ambao wananyonyesha kama ambavyo inavyofanyika kwa shule zenye mahitaji maalumu  kauli hiyo ambayo iliungwa mkono na waalimu wengi kwenye mkutano huo
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa