Home » » WATAKIWA KUFUATILIA BUNGE LA KATIBA

WATAKIWA KUFUATILIA BUNGE LA KATIBA


Na  Walter   Mguluchuma
Katavi
 Wakazi wa Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi wametakiwa kufuatilia Bunge la katiba   linaloendelea iliwaweze  kutambua yaliyomo kwenye Rasmu ya katiba  ili wawe na uamuzi sahihi  wakati wakupiga kura kwenye mikutano ya kupitisha Rasmu ya pili ya katiba
 Wito huo ulitolewa hapo juzi na mwanasheria  wa kituo na  haki za binadamu (LHRC) Fredrick  Lyimo  wakati akiwahutubia wananchi wa Mji wa Mpanda kwenye viwanja  vya maridadi  mjini hapa
 Alisema kituo  hicho  cha LHRC kitafanya mikutano kwenye Halmashauri zote za Mkoa wa Katavi  yenye lengo  la kuwahamasisha wananchi wasome rasmu ya katiba  ili yale mambo  ya muhimu yenye faida kwa watanzania  yawekwe kwenye katiba mpya
 Alifafanua  kuwa endapo wananchi watafuatilia kwa kusikiliza yanayojadiliwa na wajumbe wa Bunge la Katiba linaloendelea  watakuwa na  uamuzi sahihi wakati utakapo fika wa kupira kura ya Rasmu ya pili ya Katiba
 Lyimo  alieleza  yapo mambo ya msingi yenye faida na manufaa kwa watanzania  ambayo yanafaa kuwekwa kwenye katiba  hivyo ni vizuri wananchi wahakikishe mambo hayo yanawekwa  
 Alisema yapo  mambo mengine ambayo wananchi  watakayo yaona hayafai kwenye rasmu ya Katiba yasiyo na faida kwa Wanzania  hivyo wanayo haki ya kuyakataa kwakati wa kupiga kura ya kupitisha katiba
Nae afisa habari wa LHRC  Rose Mwalongo alieleza kuwa yapo mambo saba mapya ya kuungwa mkono  na wananchi  katika  Rasmu ya Katiba
Alitataja baadhi ya mambo hayo kuwa ni  kupanuliwa  kwa usawa wa haki za  binadamu  na wananchi kuwa na mamlaka  ya kupiga kura ya kkutokuwa na imani na Mnunge wao
Kwa upande wao wananchi  walioshiriki kwenye mkutano huo wengi wao walisema katiba ya sasa inampa Rais madaraka makubwa hivyo ni vizuri  Rais  akapunguziwa  madaraka hayo


Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa