Na Walter Mguluchuma
Mpanda Katavi
WATU kumi wamenusurika kifo baada ya gari la abiria walilokuwa
wakisafiria kuacha njia na kupinduka katika Mlima Kanono barabara ya
Tabora – Mpanda
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi , Focus Malengo akithibitisha kutokea kwa ajali hiyo amebainisha kuwa majeruhi wote wamellazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Mpanda ,mjini Mpanda kwa matibabu .
Kwa mujibu wake ajali hiyo ilitokea Jumamosi , saa 11:15
jioni kilomita 40 kutoka mjini Inyonga ambao ni Makao Makuu ya Wilaya
ya Mlele katika mkoa wa Katavi , ambayo ilihusisha gari la abiria
liitwalo , AM Bus Service aina ya Scani mali ya Mohamed Mohamed .Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi , Focus Malengo akithibitisha kutokea kwa ajali hiyo amebainisha kuwa majeruhi wote wamellazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Mpanda ,mjini Mpanda kwa matibabu .
Inadaiwa kuwa gari hilo lilikuwa likitokea mjini Tabora na kuelekea mjini Mpanda kupitia mjini Inyonga hivyo lilipofika katika Milima Kanono huku likiwa kasi kubwa dereva alishindwa kukata kona na kusababisha gari hilo kumsihinda na kuacha njai na kupindika .
“Majeruhi wote wamelazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Mpanda kwa matibabu , majina yao bado hayajafahamiaka kwa kuwa hali zao bado ni tete ambapo miongoni mwao mwanamke mmoja amevunjia mkono “ aneleza Malengo
Pia anabainisha kuwa polisi wanamsaka dereva wa gari hilo ambaye jina lake bado halijafahamika ambapo alifanikiwa kutoroka katika eneo la tukio baada ya kutokea kwa ajali hiyo na kujificha kusikojulikana .
“Uchunguzi wa awali umebainisha kuwa chanzo cha ajali hiyo ni uzembe upande wa dereva na mwendo kasi “ anaeleza Kaimu Kamanda huyo wa Polisi.Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
0 comments:
Post a Comment