Home » » WATU 2086 WALIOKUWA WAKITUMIA DAWA ZA KUFUBAZA VVU WATOROKA KWENYE VITUO VYAO VYA KUPATIWA DAWA‏

WATU 2086 WALIOKUWA WAKITUMIA DAWA ZA KUFUBAZA VVU WATOROKA KWENYE VITUO VYAO VYA KUPATIWA DAWA‏


Na     Walter   Mguluchuma 
Mpanda  Katavi
Jumla ya  watu 2086  Mkoani  Katavi   walioanzishiwa  dawa  za kufubaza  VVU  wameacha  kutumia dawa  hizo kutokana  na sababu  mbambali      baada  ya kuona  wamekuwa na  afya  njema ya kunenepa miili  yao
Hayo yalielezwa na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Katavi  Dr  Yahaya  Hussein   hivi  karibuni  wakati wa afla ya kukabidhi  pikipiki  24 kwa Halmashauri za Mkoa wa Katavi  zilizotolewa   msaada   na  shirika  la  Walter Red iliyofanyika  katika  viwanja  vya ofisi ya  Mkuu wa Mkoa wa Katavi
Alisema  Mkoa wa  Katavi  unakabiliwa  na tatizo  la utoro  wa watu  walioanzishiwa  dawa  za  kufubaza  VVU kwenye  vituo  vyao  vya  kuchukulia  dawa kwa kipindi cha zaidi ya miezi  mitatu pasipo kutowa taarifa yoyote kwenye vituo vyao walivyokuwa wakichulia dawa
Alifafanua Mkoa wa Katavi   hadi  june mwaka huu  unawatoro  2086  kati ya  watu  4187  ambao  wanatumia  dawa  za kufubaza  VVU
 Dr  Yahaya  alisema  athari kubwa  ya utoro huo  huleta  usugu  kwa dawa  zitolewazo  na hivyo kuhatarisha  uwezo wa  dawa  zitumikazo sasa  katika  siku  za usoni
Kwa kutambua hari  hiyo  jitihada  mbalimbali  zimewekwa  za kuhakikisha kilamtumiaji  wa dawa  anakuwa  na anwani sahihi  na anakuwa na msaidizi  wa kufutilia  matibabu yake
Pia  wamepanga  kuongeza  ufuatiliaji  katika ngazi ya  jamii  ambapo  mhudumu  atatumia  pikipiki  kwenda  majumbani  kufahamu  sababu ya mutumiaji wa dawa  kwanini   hakuudhuria  kituoni kwake kuchukua dawa  kadri alivyopangiwa tarehe ya kulipoti kituoni
Dr  Yahaya  alieleza  Mkoa wa Katavi  ni miongoni mwa  Mikoa  Nchini  yenye   kiwango  cha juu  cha ushamiri  wa  virusi  vya Ukimwi  ambapo  kiwango  cha  ushamiri wa VVU  katika Mkoa wa Katavi  kwa sasa ni asilimia 5.9 ukilinganishwa  naasilimia  5.1  ya  kiwango Kitaifa
Kwa upande wake mgeni Rasmi wa afla  hiyo Mkuu wa  Mkoa wa Katavi Dr Rajab Rutengwe  alilishukuru  shirika la Walter  Red kwa kutowa msaada huo wa pikipiki  24 zenye  thamani ya Tsh 52,800,000 kwa Halmashauri za Mkoa wa Katavi  ambazo zitatumika  katika  kuboresha  utoaji  wa huduma  za UKIMWI  husani  utoaji huduma za mikoba
DR  Rutengwe alisema  upatikanaji  wa pikipiki  hizi  umekuja  wakati  wakati  muafaka  ili  kuboesha  huduma  za  za  mkoba  na usafirishaji   wa sampuli  toka   kituo  kimoja kwenda  kingine  na hatimaye  ziweze  fika  mabara kuwafuatilia watoro wa  dawa 
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa