Home » » WANAFUNZI 11 WALAZWA HOSPITALINI BAADA YA KUPATA MSHITUKO WA RISASI NA MABOMU YA POLISI KUFUATIA VURUGU ZA WAFANYABIASHARA NA POLISI

WANAFUNZI 11 WALAZWA HOSPITALINI BAADA YA KUPATA MSHITUKO WA RISASI NA MABOMU YA POLISI KUFUATIA VURUGU ZA WAFANYABIASHARA NA POLISI


Na  Walter  Mguluchuma 
Mpanda   Katavi 
Wanafunzi  11 wa  Shule ya  Sekondari ya Mwangaza iliyopo  Mjini   hapa wamelazwa katika  Hospital ya Wilaya ya Mpanda baada ya kupoteza  fahamu  kufuatia Askari wa Jeshi la Polisi kufyatua Risasi   na mabomu  kwenye eneo la shule hiyo  baada ya kutokea vurugu  katika  soko la  Mpanda hoteli lililojirani baina ya polisi na wafanyabiashara wa soko hilo
Tukio   hilo limetokea  hapo jana  majira  ya  saa tano  asubuhi  katika  eneo la  shule  hiyo   lliyoko  katika  Mtaa wa  Makanyagio  mjini   hapa 
  Chanzo cha  tukio hilo ni  kwamba    Askari  mgambo wa  Halmashauri ya  Mji wa  Mpanda walikuwa wakifanya  zoezi  la kuvunjia  vibada wafanyabiasha wa Soko la  Mpanda Hoteli  ambao wamejenga  vibada  sehemu zisizositahili kitendo ambacho kilipingwa na wafabiashara wa soko hilo
Wakati askari  mgambo hao wakiwa wanaendelea na zoezi hilo huku wakiwa wamefuatana  na  Askari wawili wa jeshi la  polisi  walijaribu kutaka kuvuja kibanda cha mfanyabiashara mmoja  ambae  aliwatokea   askari hao huku  akiwa ameshikilia  panga mbili mkononi kwa lengo la kutaka kuwashambulia  askari hao huku wafanyabiashara wengine  wakiwa wameshikilia  mawe ambayo walianza kuwashambulia Askari hao
Baada ya muda mfupi Askari wa kutuliza  gasia walifika kwenye  eneo hilo la soko  na kuanza kuwashambulia wafanyabiashara waliokuwa kwenye eneo hilo bila kujali kama na wao walikuwa  kwenye vurugu hizo  pamoja  na watu waliokuwa wamefika kujipatia mahitahi hari ambayo ilifanya wafanyabiashara  wakimbie na kuacha maduka n,vibanda na meza wazi
Akisimilia tukio hilo la  hapo shuleni  Mkuu wa Shuleni hiyo Mwalimu  Simon  Lubanga  alisema  askari hao walifika  kwenye   eneo la shule yake ambayo ikojirani na soko hilo na kumkuta nje mwalimu  Joner  joseph ambae alikuwa akiongea na simu yake ya  Mkononi
Askari hao walianza kumshutumu kuwa alikuwa akitumia simu  yake  kwa ajiri  kupiga picha za tukio hilo na alikana kufanya hivyo ndipo walipompiga kwa kitako cha bunduki na kisha kunyang’anya simu yake kitendo ambachokilimfanya mwalimu huyo kutimua mbio na kuingia darasani walimokuwemo wanafunzi wa kidato cha tatu
Alisema wanafunzi wa darasa hilo walipo una mwalimu wao  amefanyiziwa kitendo hicho  walitaka kuamua kutoka nje  na wakati huo huo Askari wa kutuliza gasia walianza kufyatua risasi za baridi hewani   katika eneo la shule
Alifafanua baada ya kufyatuliwa kwa Risasi hizo  wanafunzi  mbalimbali walianza kuanguka na kupoteza fahamu kutokana  na mshituko wa   bunduki
Mkuu wa shule alisema hari ya wanafunzi ilizidi kuwa mbaya  hadi walipolazimika  kuomba usafiri wa gari la wagonjwa  la hospitali ya Wilaya ya  Mpanda  ambalo lilifika hapo lenye namba za usajiri DFP 5619  lilisaidiana  na gari la  Mbunge wa Mpanda mjini kuwawawisha  katika hospitali ya Wilaya ya Mpanda kwa matibabu
Lubanga aliwataja  wanafunzi waliolazwa  katika  Hospitali ya Wilaya ya Mpanda kuwa ni  Elizabelti  Justine  mwanafunzi wa kidato cha tatu  ambae hari yake bado sio nzuri  Milka  Geoge kidato cha nne  Winflida Masele kidato cha pili  Maria  Kasegeze kidato cha pili  Anita  Frenki kidato cha  tatu
Wengine ni   Asha  Ramadhan  Everada wanafunzi wa kidato cha pili  Merry Bukuku , Merry Bukuku   Sarafina  Mwanja na Joice Martini wanafunzi wa kidato cha pili
Lubanga alisema wanafunzi hao womelazwa katika hospitali ya Wilaya ya Mpanda katika wodi namba  tano   na hari zao huku zikiwa zinaendelea vizuri
Alisema kutokana na hari hiyo wanafunzi wa shule hiiyo wamelazimika kusitisha masomo ya siku nzima na wamerudishwa nyumbani kwao 
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa