Home » » MIUNDODUNI YASABABISHA HIFADHI YA KATAVI KUTEMBELEWA NA WATALII WACHACHE‏

MIUNDODUNI YASABABISHA HIFADHI YA KATAVI KUTEMBELEWA NA WATALII WACHACHE‏



Na   Walter   Mguluchuma 
Mpanda  Katavi
Hifadhi ya Taifa  ya   Katavi iliyoko     katika  Mkoa  wa   Katavi  inakabiliwa  na  tatizo  la kutembelewa  na   watalii wachache   ukilinganisha  na  Hifadhi za Mikoa ya Kaskazini  licha ya kujaliwa   kuwa na vivutio  vingi  na wanyama  adimu     uchache huo wa watalii unachangiwa  na  miundombinu  duni  hasa  barabara za  ndani na  nje ya Hifadhi
Hayo  yalielezwa  hapo juzi  na  Mkuu wa Idara ya   Ulinzi  wa  Hifadhi  ya  Taifa ya  Katavi Davis   Mushi   wakati  akitoa taarifa ya  Hifadhi  hiyo kwa kipindi  cha mwaka mmoja  wa 2013 na 2014  wakati wa kikao cha wajumbe wa kamati ya ushauri ya Wilaya ya Mpanda kwenye  ukumbi wa maji Mjini hapa
Alisema  Hifadhi   ya Taifa  ya  Katavi  hupokea  watalii  wastani  2000  na 3,000 kwa mwaka  huchache  huu  wa  wageni  huchangiwa  na kuwepo kwa miundombinu  duni iliyoko 
Alifafanua  miundombini  ya utalii ndani ya  hifadhi  ya  Katavi  bado  ni duni  kwani sehemu  za malazi ni chache  ukilinganisha  na mahitaji  ya  wageni  hadi hivi  sasa  kuna makampuni manne tuu binafsi  yanayotoa  huduma   ya  kupiga  mahema  kwa wageni
Mushi alieleza kuwa  kwa kipindi  cha kunzia  mwaka  2010 hadi  mwaka  2014  hifadhi ya Katavi  imetembelewa na watalii  wa kutoka  nje ya  nchi 7,462 na watalii wa ndani  7,552 na kufanya  idadi ya watalii wa  ndani na  nje waliotembelea  hifadhi hiyo kwa kipindi  cha miaka mitano kuwa ni  15,014 idadi ambayo ni ndogo  ukilinganisha  na Hifadhi nyingine
 Alisema  miundombinu  hasa ya  barabara  ya kuja hifadhi  ya Katavi ni  duni  kwani barabara  za kutoka mikoa  ya jirani  ya  Kigoma,Tabora na Rukwa  hali  inayosababisha watalii  wengi  kutofika  Katavi  ingawa kumekuwepo na jitihada  za  Serikali  za kuboresha miundombinu kwani  baadhi ya  barabara  zimeanza  kujengwa kwa kiwango cha  rami
Hifadhi  hiyo imepanga  mikakati  mbali  mbali kwa ajiri ya  kuboresha utalii  ili kuweza kufanya  hifadhi ya Katavi iweze kutembelewa na watalii wengi zaidi
Mikakati hiyo ni  kuitangaza     hifadhi  kupitia  vyombombalimbali vya  habari  na kwenye maonyesho  ya kimataifa  na kitaifa  pamoja  na kwenye  maonyesho  ya  nane  nane pia kupitia  bidhaa  mbalimbali
Alisema  Hifadhi hiyo  imepanga kuanzisha utalii wa  usiku  ili kuwawezesha watalii kuwaona  kiurasi wanyama  ambao  huwa hawaonekani  mchana  kama  vile  chui
Hifadhi ya  Taifa   ya  Katavi  ilianzishwa mwaka 1974  ikiwa     na  ukubwa kilometa  za mraba    4,471 na   inapatikana    katika Wilaya  mpya  ya  Mlele  mkoa  wa Katavi   Magharibi  mwa   Tanzania ni  hifadhi  tatu kwa ukubwa  Tanzania  baada  ya hifadhi  za Ruaha  na  Serengeti
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa