Home » » DC MAAFISA ELIMU KUWENI NA UTARATIBU UTARARIBU WA KUTEMBELEA SHULE

DC MAAFISA ELIMU KUWENI NA UTARATIBU UTARARIBU WA KUTEMBELEA SHULE


Na  Walter  Mguluchuma
Mpanda  Katavi
Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  Paza  Mwamlima  amewaagiza maafisa  Elimu  wa Wilaya hiyo  kuwa na utaratibu wa  kuzitembelea shule  za Mmsingi na Sekondari  ili waweze  kubaina changamoto zinazozikabili  shule hizo
Agizo hilo alilitowa hapo jana wakati akifungua  kikao  cha  ushauri (DCC)   cha   Halmashauri ya  Wilaya ya Mpanda kilichofanyika  kwenye  ukumbi  wa Idara  ya  maji   ulioko   mjini  hapa
Alisema  endapo  maafisa  Elimu  watakuwa  na  utaratibu  wa kutembelea  shule  zao  itawasaidia kuweza kubaini  changamoto  zinazokuwepo  kwenye shule  mbalimbali
Alieleza  zipo changamoto  mbalimbali  kwenye  shule   za Wilaya  ya  Mpanda zinazozikabili  shule  za  msingi  na  Sekondari  katika Wilaya  huyo
Mwamlimu  alisema zipo  baadhi ya  shule  na  hasa  za  msingi  zinakabiliwa  na  changamoto  za  upungufu  wa  nyumba  za waalimu na  nyingine   majengo yake yako  kwenye  hari   mbaya na  aliitolea   mfano  shule  ya  Msingi   Kabungu
Alifafanua njia  ya kutatua  changamoto hizo ni  kwa maafisa  hao  kutembelea    kwenye  shule  na wakishabaini changamoto zinazokuwepo ni lazima washirikishe wananchi  katika  kutatua  changamoto hizo
Alisema   wananchi  wa Wilaya  ya  Mpanda wako  tayari  kuchangia   shughuli  za  maendeleo   endapo viongozi  watawashirikisha  kwenye  kila  hatua  inayokuwa  imefanyika
 Alieleza  wananchi  huwa wanakuwa  wagumu  kuchangia michango  endapo  tuu pale wanapokuwa wamechangia  michango   na vingozi wanaposhindwa kuwasomea  mapato na  matumizi ya  michango  yao
Hivyo  viongozi  wanapokusanya  michango ya  Wananchi  wawe na  utaratibu  wa kuwasomea  wananchi   mapato  na  matumizi  ilikutowavunja  moyo  wananchi  za  kuchangia  michango  mbalimbali ya   shughuli  za  maendeleo

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa