Na Walter
Mguluchuma
Katavi yetu blog
Mahakama ya
Wilaya ya Mpanda Mkoa wa
Katavi imemuhukumu Emanuel Kingamkono (35) Mkazi wa Mtaa wa
Nsemlwa Mjini Mpanda
kifungo cha miaka 30 jela baada
ya kupatikana na kosa wizi wa kutumia
silaha
Hukumu hiyo ilitolewa hapo juzi na Hakimu
Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya
Mpanda Chiganga Ntengwa baada ya mahakama kulidhika
na ushahidi uliotolewa mahakamani
hapo wa upande wa utetezi na mashitaka
Awali katika
kesi hiyo mwendesha mashita Mkaguzi wa Polisi Viriginia Sodoka
aliiambia mahakama mshitakiwa alitenda kosa hilo hapo
Novemba 21 mwaka jana majira ya
saa kumi jioni katika eneo la Kijiji cha Kabatini
Siku hiyo
mshitakiwa alikuta Esta Kasajila
eneo la Kabatini akiwa na baiskeli yake huku akiwa anatafuta mahindi
mabichi kwa ajiri ya kuyanunua iliakanya biashara ya kuchoma mahindi na kuyauza
Alieleza mshitakiwa
alimweleza Esta kuwa yeye
anafahamu mahari yanapo
patikana mahindi hayo
na alimtaaka ampeleke hari ambayo ilimfanya Esta
akubalia na kufuatana nae huku
akiwa na baiskeli yake
Sodoka alidai wakati wakiwa wanaelekea huko mshitakiwa alimkaba Esta
na kumwangusha chini na kumpola
simu aina ya Nokia yenye
thamani ya Tsh 150,000 na Baiskeli yake
hata hivyo Esta alifanikiwa kuponyoka na kutimua mbio huku
akiwa akipiga mayowe ya kuomba msaada
huku Emanuel akiwa anamfuguza na
akiwa ameshikilia panga ambalo alitaka
kumkata na panga hilo lilimkosa Esta na
kung’ang’ania kwente mti
Esta alipata
msaada kwa mtu mmoja aliyekuwa akipita kwenye eneo hilo ambae nae aliungana na
Esta kupiga mayowe na watu walifika na kisha walikwenda kumtafuta mshitakiwa
lakini hawakuweza kumkuta alikuwa ameisha tokome huku akiwa amepola simu na baiskeli kwenye
eneo hilo walikuta panga ililo mkosa Esta likiwa limeng’ia kwenye mti
Alieleza baada ya
hapo mshitakiwa hakuonekana tena hadi hapo januari 14 mwaka huu walikutana na Esta kwenye Soko la matunda katika mtaa wa Kawasenje ambapo mshitakiwa aliposemeshwa na Esta alianza kutimua mbio hari ilipelekea wananchi
wamkimbize na kufanikiwa kumkamata na kumfikisha kituo cha polisi cha Mpanda
ambako toka awali tukio hilo lilikuwa
limeisha funguliwa
Mshitakiwa katika
utetezi wake aliomba mahakama imwachie
huru kwani yeye hakutenda kosa hilo na amesingiziwa tuu kwa kufananishw
Hakimu Chiganga
Ntengwa baada ya utetezi huo
alisoma hukumu kwa kuimbia mahakama kuwa kutokana na ushahidi uliotolewa mahakamani
mshitakiwa amepatikana ya kifungu
cha sheria 287 A cha kanuni ya
adhabu sura ya 16 ya
marekebisho ya mwaka 2009 hivyo mahakama
imemuhumu Emanueli Kingamkono kwenda
jela kifungo cha miaka 30 jela
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Home »
» JELA MIAKA 30 KWA NYANG'ANYI WA KUTUMIA SILAHA
0 comments:
Post a Comment