Home »
» HATARI: MTU MZIMA WA MIAKA 52 AJINYONGA KWA MTANDIO BAADA YA KUACHWA NA MKEWE
HATARI: MTU MZIMA WA MIAKA 52 AJINYONGA KWA MTANDIO BAADA YA KUACHWA NA MKEWE
Na Walter Mguluchuma
Katavi yetu Blog
Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Joseph Lukato (52) Mkazi wa kijiji cha Vikonge Kata ya Mpanda Ndogo Wilaya ya Mpanda amekutwa akiwa amejinyonga kwenye mti kwa kutumia kipande cha mtandio wa kitambaa cha nguo baada ya kupata hasira ya kuachwa na mkewe
Kwa mujibu wa Kaimu Kamanda wa jeshi la polisi Mkoa wa Katavi Focas Malengo tukio hilo lilitokea hapo julai 27 mwaka huu majira ya saa mbili asubuhi kijijini hapo katika shamba la jirani yake na marehemu
undani wa tukio wa tukio hili ni kwamba marehemu alikuwa na ugomvi wa muda mrefu na mkewe aitwaye Mary Joseph (42)aliyekuwa akimtuhumu kuwa na mausiano ya kimapenzi na mwanaume mwingine kijijini hapo
Alisema julai 19 marehemu alirudi nyumbani kwake akitokea shambani majira ya saa nane mchana na kula chakula ambacho anadai mkewe alipika chakula hicho hakikuwa kimeiva
Ndipo ulipoanza ugomvi wa wanandoa hao wawili ambapo marehemu alimtuhumu mkewe kuwa amempikia chakula kibicha kwa kuwa alichelewa kurudi nyumbani kwa kuwa alikuwa kwa mwanaume mwingine mwenye mahusiano nae ya kimapenzi
Malengo alialeza mkewe alijitahidi kujijitetea kuwa hakuwa ametoka siku hiyo nyumbani kwake na wala chakula alichompia sio kibichi bali kimeiva
Alisema hata hivyo marehemu hakukubaliana na mkewe hivyo aliendelea kumshutumu tuu mkewe na kisha alimpa kichapo
Ugomvi wa wanandoo hao uliendelea kwa muda mrefu siku hiyo na ndipo mke wa marehemu alipoamua kurudi nyumbani kwa wazazi wake kwa kuhofia usalama wa maisha yake
Marehemu alijitahidi kufanya jitihada za mara kwa mara za kumshawishi mkewe arudi nyumbani kwake ili wakaendelee kuishi kama walivyokuwa wakiishi maishayao ya mume na mke hata hivyo Mary alimkatalia katakata kurudi kwa marehemu
Alisema mke wa marehemu alipokuwa nyumbani kwao aliendelea na shughuli zake kama kawaida hadi hapo julai 27 alipewa taarifa za kifo cha mume wake kupitia kwa jirani yake na marehemu aitwaye Anton Katwana
Kaimu Kamanda Malengo alieleza mwili wa marehemu umefanyiwa uchunguzi wa kidakitari na tayari wamekabidhiwa ndugu wa marehemu kwa ajiri ya taratibu za mazishi
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
0 comments:
Post a Comment