N a Walter
Mguluchuma-Katavi yetu Blog
Mpanda Katavi
Watu
watatu wamefariki dunia hapo hapo Wilaya Mpanda Mkoa wa Katavi baada
ya gariRoli aina ya Fuso walilokuwa wakisafiria kupinduka na watu
wengine wanne wamejeruhiwa na kulazwa
katika Hospitali ya Wilaya ya
Mpanda
Ajari hiyo
ilitokea hapo juzi majira ya saa
kumi na moja jioni baada ya
gari aina ya fuso lenye
Nanba za usajiri T 168 APU lililokuwa
likiendeshwa na Dreva Deus Lukas
(28 )mkazi wa mtaa wa Kawajense Mjini hapa kupinduka katika
mlima wa Sijonga Gari mali ya mtu mmoja mkazi wa kijiji cha Ikola
alifahamika kwa jina moja tuu (MAN)
Katika hajari
hiyo watu watatu walikufa hapo hapo ambao Kamanda wa polisi wa Mkoa
wa Katavi Dhahiri Kidavashari
aliwataja kuwai ni Agnes Martin(7) mwanafunzi wa shule ya
Msingi Kashato katika Halmashauri ya mji
wa Mpanda Elizabeti Mseveni (24) mkazi wa Mtaa wa Majengo mjini Mpanda
ambae ni mama mdogo wa Agnes na Madanganya Rashid (53) mkazi wa
kijiji cha Ikola Tarafa ya Karema Wlaya ya Mpanda
Kamanda wa
Jeshi la Polisi wa Mkoa wa Katavi Dhahiri Kidavashari alisema
ajari hiyo ilitokea katika eneo la Mlima wa Sijonga Katika
Tarafa ya Kabungu Barabara
inayotoka mjini Mpanda
Kuelekea Tarafa ya Karema mwambao mwa
Ziwa Tanganyika baada ya gari hilo kukatika propelashafuti likiwa
likiwa kwenye mlima
Kidavashari
aliwataja watu wanne waliojeruhiwa ambao
wamelazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Mpanda kuwa ni
Saimoni Masafila (42)Mkazi
wa Kijiji cha Mwamapuli Tarafa ya
Mpimbwe Wilaya ya Mlele Mwasiti Juma
(19) Mwajuma Seif (19) na Nassir
Salumu mtoto mdogo wa miezi minne wote wakazi wa
mjini Mpanda
Alisema Dreva wa
gari hilo Deus Lukas alikuwa akiendesha Fuso hilo
huku akiwa amewapakia watu hao na mizigo mbalimbali ya bidhaa za
wafanyabiashara huku akiwa anatokea mjini Mpanda akiwa anaelekea katika
kijiji cha Ikola kilichoko mwambao mwa
ziwa Tanganyika
Kidavashari alifafanua
baada ya gari hilo kufika kwenye eneo la mlima wa Sijonga gari hilo
lilikatika fropela shafuti na kusababisha roli hilo kupinduka na
watu watatu walifariki Dunia hapo hapo na watu wanne walijeruhiwa na
kulazwa katika hospitali ya Wilaya ya
Mpanda wakiendelea kupatiwa matibabu
huku hari zao zikiwa zinaendelea vizuri
Alisema Dreva wa
Gari hilo alikamatwa na anaendelea
kushikiliwa na jeshi la polisi wakati taratibu za kumfikisha mahakamani
zikiwa zinaendelea ili akajibu mashitaka
ya kuhusiana na ajari hiyo
Kidavashari
alieleza mili ya marehemu wote watatu
imehifadhiwa katika chumba cha
kuhifadhi maiti katika Hospitali
ya Wilaya yaMpanda kwa ajiri ya kufanyiwa uchunguzi wa Kidaktari na baada ya
hapo watakabidhiwa ndugu kwa ajiri ya mazishi
0 comments:
Post a Comment