Home » » Mbaroni Katavi kwa kumuua dereva wa Bodaboda

Mbaroni Katavi kwa kumuua dereva wa Bodaboda

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
POLIISI wilayani Mpanda, Katavi linawashikilia watu watatu kwa tuhuma za kumuua dereva wa pikipiki ‘Bodabodai, Frank Joseph (25), mkazi wa mtaa wa Nsemlwa kwa kumchinja shigo na kisha kumpora pikipiki yake.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi, Kamishina Msaidizi Mwandamizi, Dhahiri Kidavashari, aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Charles Kidaha(29), Madia Mtema (40) na Buyenza Jendesha (40) wote wakazi wa Tarafa ya Mwese, wilayani Mpanda.
Kidavashari alisema watuhumiwa hao walimuuwa dereva wa pikipiki T 704 CDQ Sanlg, Aprili 26 mwaka huu, saa 11 jioni, eneo la Kijiji cha Mpembe.
Alisema siku ya tukio dereva huyo wa pikipiki alikuwa kwenye kijiwe chake cha kilichopo hospitali ya Wilaya ya Mpanda na alitokea mtu asiyefahamika na kumkodisha na hakuonekana hadi siku iliyofuata akiwa amemuawa na maiti yake kutelekezwa porini katika kijiji cha Mpembe.
Alisema polisi kwa kushirikiana na raia wema Mei 22 walipata taarifa kuwepo kwa watuhumiwa hao, kwani waliwasili kijijni hapo wakiwa wamepakizana kwenye pikipiki hiyo. Watuhumiwa hao wanatarajiwa kufikishwa mahakamani baada ya upelelezi kukamilika
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa