Home » » ALIYEGOMBEA UWENYEKITI WA NCCR NA JAMES MBATIA AFARIKI‏

ALIYEGOMBEA UWENYEKITI WA NCCR NA JAMES MBATIA AFARIKI‏

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Na Walter Mguluchuma
Mpanda Katavi 
Aliyekuwa mgombea  nafasi ya Mwenyekiti wa Taifa   katika  uchaguzi  wa chama cha NCCR MAGEUZI  katika uchaguzi ulipita mwishoni   mwa mwaka jana  aliyegombea na Jemes Mbatia  Charles Makofila amefariki  dunia  usiku wa kuamkia jana katika kijiji cha Mpandandogo Tarafa ya Kabungu
Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa  mjomba wake Hamadi Mapengo  ambae ni Diwani wa Kata ya Mpanda ndogo  alisema  marehemu alifariki majira ya saa nane usiku  wa kuamkia jana
Alisema marehemu alifariki  akiwa  nyumbani kwake  kutokana  na maradhi ya  ugojwa wa  homa ya matumbo   ambapo umeugua zaidi ya mwezi mmoja  na alikuwa akitibiwa katika zahanati ya kijiji hicho
Katika uhai wake  marehemu aliwahi kuwa kiongozi wa chama  hicho  ambapo  mpaka  anafariki Dunia allikuwa ni Kamishina wa mkoa wa Katavi
Pia  mbali ya kugombea  na Jemes Mbatia   nafasi ya uwenyekiti wa  Taifa  wa chama hicho  marehemu  aliwahi kuwa mgombea wa   ubunge wa jimbo la Mpanda Vijijini kupitia chama hicho  katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2010
Mjomba huyo wa marehemu alieleza kuwa marehemu Charles Makofila  atazikwa leo kwenye mababuri ya kijiji cha Mpanda ndogo majira ya saa nane   mchana

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa