Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Na Walter Mguluchuma
Mpanda Katavi
katika hariambayo haikutarajiwa waumini wa Dini ya Kislamu wanaosari katika Msikiti wa Mji wa Zamani uliopo katika mtaa wa MjiMwema Wilayani Mpanda wamepigana makonde ndani ya Msikiti kutokana na na pande mbili kupingana baini yao juu ya nani awe Imamu wa Msikiti huo
Tukio hilo la aina yake liltokea hapo Februari 21 mwaka huu majira ya saa nane mchana mara baada ya kumalizika kwa ibada ya Ijumaa iliyofanyika katika Msikiti huo iliyokuwa ikiongozwa na Shehe Hussein Mkumba
Hari ya hewa ndani ya msikiti huo ilibadirika mara baada ya swala hiyo ilipomalizika ambapo Kaimu Shehe Mkuu wa Mkoa wa Katavi Ally Hussein ambae pia ndiye shehe mkuu wa wilaya ya Mpanda aliposimama na kuwaeleza waumini hao kuwa hatua inayofuata ni ya kumkabidhi hati ya Uimamu mpya wa msikiti huo Yassin Kasote
Baada ya kuuli hiyo Shehe Ally Hussen alianza kusoma hati hiyo kitendoambacho kiliwaudhi baadhi ya waumini hao ambao hawakubaliana kuongozwa na Imamu Yassin Kasote ambaye alichaguliwa hivi karibuni katika uchaguzi uliofanyika Januari 29 baada ya kumshinda mgombea mwenzake wa nafasi hiyo Muajiri Mzee
Wakati akiendelea kusoma hati hiyo kundi hilo linalompinga Kasote liliokuwa likiongozwa na Ally Kibauka Mawisa walikwenda kufunga milango ya misikiti huo na kutangaza kuwa atoki mtu humo ndani
Baada ya kufunga milango walimfuate Kasote wakimtaka awapatie hati ambayo alikuwa amekabidhiwa na viongozi wa Bakwata waliokuwa wameongozwa na Kaimu shehe wa Mkoa wa Katavi kitendo ambacho Kasote kakukubaliana nacho
Shehe Kasote alipoona anataka kupolwa hati hiyo alianza kuwashambulia kwa makonde hari ambayo iliwafanya waumini wanao muunga mkono nao kuungana nae hari ambayo ilisababisha mapingano kuanza baina ya pande hizo mbili
Hata hivyo wakati mapingano yakiwa yanaendelea baadhi ya waumini waliokuwa ndani ya msikiti huo wakiwemo askari polisi wa Dini hiyo waliweza kufanikiwa kufungua milango ya msikiti huo na kufanikiwa kumaliza vurugu hizo na kisha makundi hayo yote mwawli walikwenda kituo cha polisi cha mpanda mjini kutoa taarifa kuhusiana na vurugu hizo
Kwa upande Kaimu Shehe Mkuu wa Mkoa wa Katavi Shehe Ally Hussen amewaomba waumini wa Dini hiyo ya Kisramu wawe na utelivu wakati wa kipindi hiki cha mgogoro huo
Amesema kikubwa anachotaka waumini wa Dini hiyo ni kuhakikisha wanaendeleza amani katika msikiti huo sio kuleta machako ndani ya msikiti na nje ya msikiti
Nae mmoja wa kundilinalompinga Imamu mpya alisema wao hawakotayari kuongozwa na Imanu Yassin Kassote kutokana na uchaguzi uliofanyika wa kumchagua ulikiuka taratibu za katiba yao
Jeshi la polisi Mkoa wa Katavi limekiri kuwepo kwa vurugu kwenye ibada hiyo siku hiyo ya tukio katika msikiti huo wa Mji wa Zamani
0 comments:
Post a Comment