Home » » zaidi ya wanafunzi elfu tano hawajuwi kusoma, kuandika na kuhesabu‏

zaidi ya wanafunzi elfu tano hawajuwi kusoma, kuandika na kuhesabu‏

 
 Katibu Tawala Mkoa wa Katavi Eng. Emmanuel Kalobelo akifubgua mafunzo
ya siku mbili ya utafiti wa wanafunzi  wasio jua kusoma , kuandika na
kuhesa katika ukumbi wa Kanisa Katoliki Jimbo kuu la Mpanda.
Picha na Walter Mguluchuma
 
Na  Walter Mguluchuma
Mpanda  -Katavi yetu Blog
Zaidi ya wanafunzi elfu tano wanaosoma katika shule za msingi katika
Mkoa wa  Katavi wakiwa  wanasoma darasa  la pili hawajuwi kusoma
kuandika na kuhesabu
Hayo yalisemwa hapo juzi  na Katibu  Tawala wa Mkoa wa Katavi Mwandisi
 Emanuel  Kalobelo wakati akifungua  mafunzo  ya siku  mbili  ya
utafiti  wa matokeo  ya ujifunzaji  kwa  watoto  wa miaka  saba  hadi
miaka kumi na sita  yaliyofanyika katika ukumbi wa Kanisa Katoriki
jimbo la Mpanda
Mafunzo hayo yaliyo  andaliwa na shirika  lisilo la Kiserikali
linaloitwa  (UWEZO TANZANIA)   yanawashirikisha washiriki  kutoka
Halmashauri zote zilizopo katika Mkoa wa Katavi ambazo ni Halmashauri
ya Mlele, Nsimbo, Mpanda na Halmashauri ya Mji wa Mpanda
Mwandisi Kalobelo alisema kuwa Mkoa wa Katavi  unajumla ya wanafunzi
5,855 ambao hadi sasa wanao soma darasa la pili  wakiwa hawajuwi
kusoma kuandika na kuhesabu
Alisema lengo la  Mkoa wa Katavi ni kuhakikisha kwamba wanafunzi
wanajua  kusoma  na kuandika  wakiwa Darasa la pili
Pia alisema  mkoa umepanga  kuinua  ufaulu  wa mitihani wa kumaliza
elimu ya  msingi  kufikia  asilimia 60%  mwaka huu  ambapo  ufaulu wa
mwaka jana kwa wanafunzi  wa darasa la saba ulikuwa ni asilimia 26%
Alifafanua kwa shule za Sekondari  wamepanga kuinua ufaulu  wa mtihani
wa kidato cha nne  kufikia asilimia 60% mwaka 2013 kutoka asilimia 42%
za mwaka 2012 na asilimia 70%  mwaka 2014 na asilimia  80%  mwaka 2015
Alisema ili kufikia malengo hayo Mkoa umepanga  mikakati  wa upangaji
wa shule kuwa  katika madaraja  na kutangaza matokeo ya mitihani ya
kila shule  kwenye  vyombo vya habari  na mbao za matangazo pamoja na
kutowa tuzo kwa shule zinazofanya vizuri
Mikakati mingine ni  kutowa motisha kwa walimu ,kuwapa mafunzo ya mara
kwa mara waalimu ,kuwepo  kwa ruzuku  ya uendeshaji  wa shule  na
ujenzi  wa miundombinu  muhimu  ya shule
Kalobelo alizitaja changamoto zinazoikabili  sekta  ya elimu  katika
Mkoa wa Katavi  ni utoro wa wanafunzi, uhaba  wa miundombinu  kama
vile nyumba za walimu,  vyumba vya madarasa  na matundu ya vyoo
Changamoto nyingine ni upungufu wa walimu hasa wa shule za sekondari
kwani waliopo  kwa sasa ni 762 ambao ni sawa na  asilimia 68%  wakati
mahitaji ya walimu wa shule za sekondari ni 1,121 pia bado kuna tatizo
 la uhaba  wa vifaa vya kujifunzia na kufundishia
Kwa upande wa shule za msingi  waliopo ni asilimia 96% tatizo lililopo
ni  walimu  kupangwa bila kuzingatia mahitaji ya  waalimu  kwani shule
nyingine zimekuwa zikipangiwa waalimu waalimu wengi bila kujali
mahitaji yao hivyo ameziagiza Halmashauri zote za Mkoa wa Katavi
kupanga waalimu kwa kuzingatia mahitaji
Kwa upande wake Mratibu wa  UWEZO wa Mkoa wa Katavi Godfrey Mogellah
alisema mafunzo hayo  yamekuwa yakifanyika kwa  kipindi cha miaka
minne sasa  katika nchi tatu za Tanzania , kenya na Uganda na mwaka
huu mafunzo hayo yanafanyika kwa wilaya 133 hapa nchini
Alisema mara baada ya kupata mafunzo hayo  watafanya utafiti  kwenye
shule mbalimbali na kwenye mitaa na vitongoji ili kuweza kuwabaini
wanafunzi walioko mashuleni na majumbani ambao hawajuwi kusoma,
kuandika na kuhesabu

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa