Home » » HOT NUUUZ: TAKUKURU YAMFIKISHA MAHAKAMANI MWENYEKITI WA BARAZA KWA RUSHWA YA NGONO‏

HOT NUUUZ: TAKUKURU YAMFIKISHA MAHAKAMANI MWENYEKITI WA BARAZA KWA RUSHWA YA NGONO‏

Na Walter Mguluchuma
Mpanda Katavi
Taasisi ya kuzuia  na kupambana  na Rushwa  Mkoa wa Katavi imemfikisha mahakamani  mwenyekiti  wa Baraza la Kata ya Kapalala Tarafa ya Nsimbo  Wilaya ya Mlele Mkoani hapa  Salvatory Mwanakatwe (63) kwa tuhuma za kuomba Rushwa ya ngono
Kwa mijibu wa mkuu wa Takukuru Mkoa wa Katavi John Minyenya  mtuhumiwa  anadaiwa kutenda kosa hilo  mnamo  Agosti 11 mwaka juzi katika nyumba ya kulala wageni  inayoitwa Mawenzi iliyoko katika mtaa wa mji mwema
Mtuhumiwa anadaiwa akiwa mwenyekiti wa Baraza la Kata alitumia wadhifa wake  kutenda kosa  la kumshawishi  na kumwomba Rushwa ya ngono  mwanamke mmoja ambae jina limehifadhiwa  ili  amsaidie  katika  shauri lake dhidi ya mumewe ambae alikuwa amemshitaki kwenye Baraza hilo  kwa kumtelekeza  na kisha kuuza mali walizochuma pamoja
Minyenya alieleza mbele ya waandishi wa habari kuwa mwanamke huyo baada ya kuombwa Rushwa hiyo ya ngono akuridhika na kitendo hicho cha kutoa rushwa ya ngono kwa mwenyekiti wa Baraza la Kata
Alisema ndipo alipofikisha taarifa kwenye Taasisi  ya kupambana na Rushwa Mkoani Katavi kuhusiana na tuhuma  za  Salvatory Mwanakatwe  kudai apewe  Rushwa ya ngono na mwanamke huyo
TAKUKURU  baada ya kupokea taarifa hizo  ilianza kufanya  uchunguzi  juu ya rushwa hiyo  ya ngono  na iliweza kubaini kuwa tuhuma hizo zilizotolewa na mwanamke huyo  ni za kweli
Alisema ndipo Maafisa wa TAKUKURU  walipoandaa mtego wa Rushwa dhidi ya mshitakiwa Salvatory  hapo mnamo Agosti 11  2011 na kufanikiwa kumkamata  mtuhumiwa akiwa kwenye nyumba ya kulala wageni ya Mawenzi Katika mtaa wa Mji Mwema akiwa na mwanamke huyo
Mshitakiwa  amefikishwa mahakamani  na kusomewa  shitaka la kuomba rushwa ya ngono  ikiwa ni kinyume  na kifungu cha sheria  cha 25  cha sheria ya  kuzuia  na kupambana  na Rushwa namba 11ya  mwaka 2007 
Mshitakiwa  baada ya kusomewa mashitaka  yanayomkabili dhidi yake  alikana kutenda kosa hilo  hata hivyo mtuhumiwa alikwenda rumande baada ya kushindwa kutimiza masharti ya dhamana
Mkuu wa Takukuru wa Mkoa wa Katavi alieleza kuwa kesi hiyo imechelewa kufunguliwa  kutokana na taratibu zilizopo sasa ambapo  kesi zote zinazofunguliwa na Takukuru mahakamani lazima kibali kitoke kwa mwanasheria mkuu wa Serikali
Aidha TAKUKURU imetowa  wito kwa wananchi  wote kuzingatia  maadili  na kutojihusisha  na vitendo vya  Rushwa  wakati wa kutekeleza majukumu yao  ya kila siku wakati  wanapodai  haki zao kwani Rushwa ni adui  wa haki  hivyo  Rushwa  haikubaliki

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa