Home » » WATANO WASHIKILIWA NA POLISI BAADA YA KUPATIKANA NA VINYWAJI VINAVYODHNIWA KUWA NA MADAWA YA KULEVYA‏

WATANO WASHIKILIWA NA POLISI BAADA YA KUPATIKANA NA VINYWAJI VINAVYODHNIWA KUWA NA MADAWA YA KULEVYA‏

Na Walter Mguluchuma
Mpanda
jeshi la  polisi Mkoa waKatavi linawashikilia watu watano kwa  tuhuma za kapatikana na vinywaji   aina juice  Grand malt  na pipi  zikiwa zimechanganywa madawa ya kulevya
Kamanda wa polisi wa Mkoa wa Katavi Dhahiri Kidavashari aliwataja waliokamatwa kuwa ni  Halid  Bukela (38) mkazi wa  Area C  Dodoma,  Mayala Udembi( 45)  mkazi wa mtaa wa Kigamboni  Mpanda, Adulofu Kajuna (35)   mkazi wa  Nyamagana   Jijini Mwanza,   Lucas Damiani   (24) na  Elias  Daudi (34 ) wote wakazi wa   Wilaya ya Urambo Mkoa wa Tabora.
Watuhumiwa hao walikamatwa  juni  5 majira ya saa  10  jioni katika Mtaa wa Majengo B’  Wilayani Mpanda   wakiwa  na  pipi moja  juice  mbili    na Grand  Malta   moja  ambazo zilikuwa  zimechanganywa madawa ya kulevya  ambapo  katika  tukio  hilo walikamatwa  wahumiwa  wawili  Halidi  na Maloda
Kidavashari  alisema watuhumiwa walikamatwa  kufutia taarifa ambazo zilikuwa zimelifikia jeshi la polisi kuwa watumiwa wanajihusisha na  vitendo  vya  utapeli    na wanawalevya  watu kwa madawa ya kulevya  na kisha  wanawaibia mali zao
Alisema baada ya watuhumiwa  kukamatwa  na kuhojiwa  na Polisi walibaini  kuwa watuhumiwa hao walikuwa wakishirikiana na  wenzao  ambao  walikuwa katika Kijiji cha Kakese  na ndipo Polisi walipo fanikiwa kuwakamata watu  hao watu
Watuhumiwa hao  ambao ni   Adolofu   Lucas na Elias  huku wakiwa na pipi  inayodhaniwa kuwa na  dawa  za kulevya
Kamanda Kidashari alisema  watuhumiwa hao wote watano  bado wanaendelea kushikiliwa  na jeshi la polisi  kwa mahojiano zaidi  na watafikishwa Mahakamani  baada ya uchunguzi kukamilika
Mkoa wa Katavi umekuwa  ukikabiliwa na matukio mbali mbali  ya utapeli hivi karibuni kutokana  na kuongezeka kwa wafanya biashara  wanaotoka nje ya Mkoa huu   kwa ajili ya kununua mazao ya Nafaka aina ya  mpunga,  mahindi  na ufuta 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa